JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
Simu: 022-2121600 Faksi: 022-2113271 Tovuti: www.moe.go.tz
TANGAZO KUHUSU NAFASI ZA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA CHETI NA STASHAHADA KWA MWAKA WA MASOMO 2012/2013
NB: MWISHO WA KUPOKEA BARUA ZA MAOMBI NI TAREHE 30/04/2012.
Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi anatangaza nafasi za mafunzo ya ualimu ngazi ya Cheti na Stashahada kwa mwaka wa masomo 2012/2013 kama ifuatavyo:
(A) MAFUNZO YA UALIMU TARAJALI NGAZI YA CHETI
1. CHETI DARAJA A: MUDA WA MAFUNZO NI MIAKA 2
Mwombaji awe na sifa zifuatazo:
(a) Aliyehitimu Kidato cha 4 kati ya mwaka 2009 hadi 2011 na kufaulu katika kiwango kisichopungua daraja la IV alama 27 kwa mtihani uliofanyika katika kikao kimoja AU mwenye ufaulu wa masomo manne kwa kiwango cha C au zaidi (masomo yanayofundishwa katika shule za Msingi) kwa mitihani iliyofanyika katika vikao zaidi ya kimoja;
(b) Aliyehitimu Kidato cha 6 na kukosa sifa za kujiunga na Stashahada ni sifa ya nyongeza.
Kipaumbele kitatolewa kwa waliofaulu masomo ya ‘Mathematics, Biology, Physics, Chemistry and English‟.
2. CHETI (MICHEZO): MUDA WA MAFUNZO NI MIAKA 2
Mwombaji awe na sifa zifuatazo:
(a) Ufaulu wa Kidato cha 4 kwa kiwango kisichopungua daraja la IV alama 27 (Kipaumbele kitatolewa kwa waliofaulu masomo ya ‘Mathematics, Biology, Physics, Chemistry and English‟;
(b) Aliyehitimu Kidato cha 6 na kukosa sifa za kujiunga na Stashahada ni sifa ya nyongeza; na
(c) Mwenye uzoefu katika michezo ni sifa ya nyongeza (vithibitisho viambatishwe).
3. CHETI (ELIMU YA AWALI): MUDA WA MAFUNZO NI MIAKA 2
Mwombaji awe na sifa zifuatazo:
(a) Aliyehitimu Kidato cha 4 kati ya mwaka 2009 hadi 2011 na kufaulu katika kiwango kisichopungua daraja la IV alama 27 kwa mtihani uliofanyika katika kikao kimoja; na
(b) Kuhitimu Kidato cha 6 ni sifa ya nyongeza.
(B) MAFUNZO YA WALIMU KAZINI NGAZI YA CHETI
1. CHETI SAYANSI KIMU: MUDA WA MAFUNZO NI MWAKA 1
Mwombaji awe na sifa zifuatazo:
(a) Mwalimu kazini aliyepitia mafunzo ya ualimu Daraja A;
(b) Uzoefu wa kazi ya ualimu usiopungua miaka 2;
(c) Aliyefaulu masomo ya Sayansi na Sayansi Kimu; na
(d) Aliyefaulu mtihani wa Kidato cha 4 kwa kiwango kisichopungua daraja la IV alama 28.
2. CHETI ELIMU MAALUM: MUDA WA MAFUNZO NI MWAKA 1
Mwombaji awe na sifa zifuatazo:
(a) Mwalimu kazini aliyepitia mafunzo ya ualimu Daraja A;
(b) Uzoefu wa kazi ya ualimu usiopungua miaka 2;
(c) Aliyefaulu angalau somo moja la Sayansi katika mtihani wa Kidato cha 4;
(d) Aliyefaulu mtihani wa Kidato cha 4 kwa kiwango kisichopungua daraja la IV alama 28; na
(e) Mwalimu anayefundisha Elimu Maalum hata kama hana mafunzo rasmi ni sifa ya nyongeza(vithibitisho viambatishwe)..
(C) MAFUNZO YA UALIMU TARAJALI NGAZI YA STASHAHADA
1. STASHAHADA YA UALIMU MASOMO YA SAYANSI, SAYANSI YA JAMII NA LUGHA : MUDA WA MAFUNZO NI MIAKA 2
Mwombaji awe na sifa zifuatazo:
Ufaulu wa Kidato cha 6 kwa kiwango kisichopungua „Principal Pass‟ moja na „Subsidiary‟ moja za masomo yanayofundishwa katika shule za sekondari Kidato cha 1 hadi 4.
Masomo yanayofundishwa katika shule za sekondari Kidato cha 1 hadi 4 ambayo ni; Mathematics, English, Kiswahili, History, Geography, Civics, Biology, Chemistry, Physics, Agricultural Science, Bookeeping, Commerce.
2. STASHAHADA YA UALIMU MICHEZO, MUZIKI, SANAA ZA UFUNDI NA SANAA ZA MAONESHO: MUDA WA MAFUNZO NI MIAKA 2
Mwombaji awe na sifa zifuatazo:
Ufaulu wa mtihani Kidato cha 6 kwa kiwango kisichopungua „Principal Pass‟ moja na „Subsidiary‟ moja kwa kuzingatia masomo yafuatayo kwa kila kozi:
-Sanaa za Ufundi: masomo ya ‘Fine Art’ pamoja na ufaulu wa Kidato cha 4 masomo ya ‘Biology, History, Physics, English, and Civil Engineering’
-Sanaa za Maonesho: masomo ya ‘Literature in English, Kiswahili, Geography and History;
-Muziki: masomo ya ‘English, Kiswahili, Music, Physics, Geography and History’; na
-Elimu kwa Michezo: masomo ya Biology, Chemistry, Physics, English’ na Kiswahili.
3. STASHAHADA YA UALIMU UFUNDI: MUDA WA MAFUNZO NI MIAKA 2
Mwombaji awe na sifa zifuatazo:
(a) Mwenye cheti cha FTC kutoka vyuo vya Ufundi (Arusha, Mbeya, Dar es Salaam) au sifa zinazolingana; na
(b) Mwenye umri usiozidi miaka 35.
4. STASHAHADA YA UALIMU KILIMO: MUDA WA MAFUNZO NI MIAKA 2
Mwombaji awe na sifa zifuatazo:
Ufaulu wa mtihani Kidato cha 6 kiwango kisichopungua “Principal Pass” moja na “Subsidiary” moja katika somo la ‘Agricultural’ Science na ‘Biology’ au ‘Chemistry’.
5. STASHAHADA YA UALIMU BIASHARA: MUDA WA MAFUNZO NI MIAKA 2
Mwombaji awe na sifa zifuatazo:
Ufaulu wa mtihani wa Kidato cha 6 kwa kiwango kisichopungua „Principal Pass‟ moja na „Subsidiary‟ moja za masomo ya ‘Accounts and Commerce’.
6. STASHAHADA YA UALIMU SAYANSI KIMU: MUDA WA MAFUNZO NI MIAKA 2
Mwombaji awe na sifa zifuatazo:
Ufaulu wa mtihani wa Kidato cha 6 kiwango kisichopungua ‘Principal Pass‟ moja na „Subsidiary‟ moja katika masomo ya ‘Biology, Chemistry and Nutrition’.
(D) MAFUNZO YA WALIMU KAZINI NGAZI YA STASHAHADA
1. STASHAHADA YA UALIMU MASOMO YA SAYANSI, SAYANSI YA JAMII NA LUGHA: MUDA WA MAFUNZO NI MIAKA 2
Mwombaji awe na sifa zifuatazo:
(a) Mwalimu mwenye Cheti cha Ualimu Daraja A na uzoefu kazini usiopungua miaka miwili; na
(b) Ufaulu wa mtihani Kidato cha 6 kwa kiwango kisichopungua ‘Principal Pass‟ moja na „Subsidiary‟ moja za masomo yanayofundishwa katika shule za sekondari (Kidato cha 1 hadi 4). Masomo yanayofundishwa katika shule za sekondari ni; Mathematics, English, Kiswahili, History, Geography, Civics, Biology, Chemistry, Physics, Agricultural Science, Bookeeping, Commerce.
2. STASHAHADA YA UALIMU ELIMU MAALUM: MUDA WA MAFUNZO NI MIAKA 2
Mwombaji awe na sifa zifuatazo:
(a) Mwalimu mwenye Stashahada ya Ualimu fani ya Sayansi au Sayansi ya Jamii na uzoefu kazini usiopungua miaka miwili ;
(b) Ufaulu wa mtihani wa Kidato cha 6 kwa kiwango kisichopungua „Principal Pass‟ moja na „Subsidiary‟ moja za masomo yanayofundishwa katika shule za sekondari;
(c) Mwalimu anayefundisha watoto wenye mahitaji maalumu (wasioona, viziwi, wenye ulemavu wa akili nk) ni sifa ya nyongeza (vithibitisho viambatishwe).
3. STASHAHADA YA UALIMU SAYANSI KIMU: MUDA WA MAFUNZO NI MIAKA 2
Mwombaji awe na sifa zifuatazo:
(a) Mwalimu mwenye Cheti cha Ualimu Daraja A;
(b) Mwalimu mwenye Cheti cha ualimu Sayansi Kimu; na
(c) Ufaulu wa mtihani wa Kidato cha 6 kwa kiwango kisichopungua ‘Principal Pass‟ moja na „Subsidiary‟ moja za masomo ya ‘Biology, Chemistry and Nutrition’.
VIAMBATISHO/ MAELEZO MUHIMU
Waombaji wa mafunzo ya Ualimu waambatishe vielelezo vifuatavyo:
(i) Nakala za vyeti vya ufaulu Kidato cha IV na cha VI;
(ii) Nakala za vyeti vya kuhitimu mafunzo ya ualimu ngazi ya Cheti na Stahshahada (kwa Walimu kazini);
(iii) Barua za Walimu kazini zilizopitishwa na Waajiri;
(iv) Sifa zilizoelekezwa kwa kila kozi ni kwa ajili ya waombaji wa mafunzo ya ualimu katika vyuo vya ualimu vya Serikali na Vyuo Visivyo vya Serikali;
(v) Wahitimu wa Kidato cha 4 mwaka 2011 na Kidato cha 6 mwaka 2012 walioomba kupitia „Sel forms‟ wanatakiwa kutuma maombi upya kwa barua;
(vi) Majibu kwa watakaochaguliwa kujiunga na mafunzo ya ualimu yatatolewa kwenye Tovuti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi;
(vii) Barua za kujiunga na mafunzo zitatolewa na chuo atakakopangwa mwombaji kwa kutumia anuani ya yake; na
(viii) Tangazo hili lipo pia katika tovuti ya Wizara: www.moe.go.tz, Ofisi za Makatibu Tawala (M) na Vyuo vya Ualimu.
MWISHO WA KUPOKEA BARUA ZA MAOMBI NI TAREHE 30/04/2012.
Maombi yatumwe kwa:
KATIBU MKUU,
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI,
S.L.P. 9121,
DAR ES SALAAM (Aione: Mkurugenzi, Elimu ya Ualimu)
Kumekuwa na maswali lukuki watu wakitaka kujua nini maana ya mean Test kama zinavyotolewa na BODI ya mikopo ya Elimu ya juu. Fuatana na makala haya kuelewa zaidi:
4.1 Means Testing System
The Board has since 2011/2012 academic year reviewed the Means testing system to make it Simple, Transparent and Fair. The Means Testing System considers School Fees paid in O – level, A – Level Secondary Schools or Ordinary Diploma as indication of applicant's ability to contribute to the costs of higher education.
Thus, Applicant's neediness shall be measured as a difference between the higher education costs (Meals and Accommodation charges, Books and Stationery expenses, Special Faculty Requirement expenses, Field Practical expenses, Research expenses and Tuition Fees) of a particular institution of study and the applicant's ability to pay for his/her own education; multiplied by a factor to acknowledge the high return of Higher Education to the applicant. The factor ranges from 1.1 to 1.5 depending on the magnitude of Tuition Fees paid at O-Level and A-Level Secondary/Ordinary diploma Education. The higher the magnitude, the higher the factor.
In addition, the system shall make adjustments to cover for Loan applicants with special socio-economic disadvantages such as Orphanage, Disability (of Parents/applicants) and Single parency.
Underthe new Means Testing System, the whole loan shall be aggregated to one lump sum amount. Out of that, the Tuition Fee and Special Faculty Requirement components shall be paid directly to the Institution of study, whereas the remaining amount shall be paid to the student quarterly.
The Means Test shall be applicable to first time applicants on Tuition fee and Special Faculty Requirements loan items only. The other four loan items meals and Accommodation, Books and Stationery, Field Practical Training and Research may be allocated one hundred (100) per cent loans.
4.2 Coverage of the Means Testing System
The new means test system shall be applicable to the first time loan applicants in the 2012/2013 academic year and subsequent years who will be admitted to pursue all programmes that will not be eligible for 100% loans.
4.3 Number of Students to be Granted Loans
In view of limited loanable funds budget, and pursuant to section 7 paragraph (1) of Act No 9 of 2004 (as amended), the Board in 2012/2013 academic year shall issue loans to a limited number of applicants as per allocated budget. In view of limited loanable funds budget, candidates who are able to meet costs for higher education, are strongly advised not to apply for loans from the Board.
4.4 Award of One Hundred Per-cent (100%) Loans
To motivate candidates to join professions which currently have critical shortages, the following programmes shall be awarded up to one hundred (100%) per cent loans:-
4.4.1 Health Sciences as defined in section 3.7.2 above.
4.4.2 Bachelor of Education with Science, Bachelor of Science with Education and Bachelor of Education (Mathematics).
4.4.3 Irrigation Engineering.
4.5 Candidatesadmitted into Education Non- Science and Non Mathematics Education Programmes.
Candidates admitted into education programmes which are non- science and non mathematics education programme shall be eligible for Means Tested loans of not less than fifty (50%) per cent.
(Kisha fuata maelekezo )
NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo ameamuru kukamatwa na kushitakiwa kwa wakuu wa shule 10 za sekondari mjini Kigoma Ujiji ambao wamebainika kuruhusu wanafunzi 391 waliofeli mitihani yao ya kumaliza elimu ya msingi, kuendelea na masomo ya sekondari.
Mulugo alisema hayo kwa nyakati tofauti akiwa katika ziara ya siku mbili mkoani hapa na kuongeza kuwa baada ya hatua ya awali ya kuwavua madaraka ya ukuu wa shule na uchunguzi kufanywa na tume mbalimbali, imethibitika kuwa wakuu hao walihusika na vitendo hivyo.
Alisema walifanya vitendo hivyo kinyume na Sheria ya Elimu namba 25 ya mwaka 1978 na marekebisho yake ya mwaka 2002, huku wakijua vitendo hivyo ni kosa kwa mujibu wa sheria za uendeshaji shule za sekondari.
Akizungumza katika sekondari ya Kasingirima, Naibu Waziri alisema kuwavua madaraka ilikuwa ni hatua ya awali ya kinidhamu.
Baada ya hapo, kinachofuata ni kuchukuliwa hatua za kisheria kwa sababu vitendo vilivyofanyika vya kuwadahili wanafunzi wasio na sifa kuendelea na masomo ya sekondari katika mfumo rasmi wa Serikali, ni kinyume cha sheria.
"Hapo kwa haraka haraka kuna makosa mawili tayari yametendeka; moja ni kughushi nyaraka halali za Serikali na kuwaingiza wanafunzi hao, lakini la pili ni vitendo vya rushwa ambavyo vinaonekana kutendeka katika kuwaingiza wanafunzi hao," alidai.
Katika ziara yake jana mjini Kigoma, Mulugo alitembelea shule tano za sekondari zinazotuhumiwa kuhusika na kadhia hiyo ambazo ni Kasingirima, Mwananchi, Katubuka, Masanga na Mlole. Pia alitembelea Chuo cha Ufundi Stadi (Veta) na jioni alikwenda katika mkutano wa majumuisho na viongozi mbalimbali.
Sambamba na ziara katika maeneo hayo pia, Mulugo anatarajia kuwa na mkutano wa hadhara katika viwanja vya Mwanga Centre ambapo pamoja na mambo mengine alipanga kuwaeleza wazazi madhara ya kuwaingiza katika mfumo rasmi wanafunzi waliofeli mitihani ya kumaliza elimu ya msingi.
Mkuu wa Shule ya Sekondari Kasingirima, Nkanuliye Hamisi, alikanusha kuhusika na kuwaingiza wanafunzi na kujipatia fedha akidai kuwa alishangazwa na kuwapo kwa wanafunzi hao baada ya kufanyika ukaguzi kutoka nje na kuwa jambo hilo lilifanywa kinyemela kwa wanafunzi kuingia bila kusajiliwa.
Hata hivyo, Elisha Zilikana ambaye ni Mkuu wa Shule ya Sekondari Mwananchi, alikiri kuhusika kuingiza sekondari wanafunzi waliofeli mitihani yao ya darasa la saba akidai kuwa jambo hilo lilifanyika kutokana na huruma kwa watu wanaomzunguka huku akiomba kupewa msamaha kutokana na jambo hilo.
Mwishoni mwa mwaka jana, Ofisi ya Mkaguzi wa Sekondari Kanda ya Ziwa Magharibi ilifanya ukaguzi na kugundua uwepo wa wanafunzi 391 wanaoendelea na masomo ya sekondari wakati walifeli masomo yao ya shule za msingi.
Shule hizo za sekondari zilizokumbwa na kadhia hiyo ni pamoja na Mwananchi, Kasingirima, Rusimbi, Kitongoni, Katubuka, Buteko, Wakulima, Mlole na Masanga ambapo wanafunzi waliokuwa wakisoma katika shule hizo, walilazimika kusitisha na masomo.
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kushirikiana na Baraza la Mitihani Taifa (Necta)
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kushirikiana na Baraza la Mitihani Taifa (Necta), imesema kuwa itafanyia marekebisho baadhi ya sheria zinazolihusu baraza hilo ili kulipa meno ya kuwawajibisha moja kwa moja watu wanaohusika na kughushi vyeti na udanganyifu wa mitihani.
Kauli hiyo imetolewa na Afisa Elimu wa Mkoa wa Dodoma, Remigius Ntyama kwa niaba ya Naibu Waziri wa wizara hiyo, Philipo Mulugo, katika mahafali ya chuo cha ualimu cha Capital. Alisema baadhi ya sheria zilizopo zimekuwa zikilifanya Baraza hilo kukosa meno ya kuwawajibisha watu wa aina hiyo.
Ntyama alisema, utaratibu wa hivi sasa wa baraza mara baada ya kubainika kwa vyeti vya namna hiyo, chuo husika ndicho kinachoachiwa kazi ya kuchukua hatua. Hata hivyo, alisema hali hiyo imekuwa ikitoa mwanya kwa wahusika kutoroka.
Alieleza kuwa suala la Baraza kuchukua hatua amelichukuwa na utaratibu utawekwa ili liwe ndiyo lenye uwezo wa kuchukua hatua mara linapogundua kuwa cheti kimeghushiwa.
Kwa upande wa Mkuu wa chuo hicho, Khan Nassor Charokiwa, alisema utaratibu wa uhakiki wa vyeti vya wanachuo unaofanywa na baraza hilo umekuwa ukiondoa dhana nzima ya zoezi hilo kwani lengo la kupeleka vyeti kwa uhakiki baraza ili kubaini vilivyohalali hurudisha kesi kwa vyuo kuwa hawafanyi kazi vizuri. Alisema hali hiyo ni kuwaonea kwani vyeti vya taaluma ya sekondari anayeweza kuvichambua vema ni Baraza na sio mtu mwingine yeyote.
Mkuu huyo alisema changamoto hiyo inatokana na kutokuwa na ofisi za Baraza la mitihani kanda ambapo kungetoa nafasi kubwa kwa vyuo hivyo ambavyo vipo mikoani kusafirisha vyeti ni tatizo hasa ikitokea upotevu au ajali. Pia alitoa ombi kwa serikali kusitisha badiliko la sifa za udahili kwa mwaka huu kutoka pointi 28 hadi 27 katika kozi ya ualimu.
Alisema wao kama chuo wanaelewa umuhimu wa kuongeza sifa za kujiunga ili wapatikane walimu bora lakini kabla ya kupata waraka wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Machi 13, 2012 tayari walikuwa wameshatangaza na kupokea maombi ya wanafunzi mara baada ya matokeo ya kidato cha nne. Alieleza kuwa mabadiliko hayo yamekuja ghafla wakati watanzania wengi ufaulu wao haukuwa mzuri hasa wale waliosoma shule za kata kutokana na mazingira ya shule hizo.
Tumejaribu kuchukua mambo muhimu yaliyomo kwenye mwongozo wa TCU, lakini unaweza kugonga
hapa ili u-download full guide book. Kwa wasio fahamu website ya TCU, ni
www.tcu.go.tz ambapo unaweza kusoma na kuelewa pamoja na ku-apply online.
Yafuatayo ni baadhi tu ya machache ambayo tumeyachukua, kwa msaada zaidi wasiliana na TCU/NACTE:
1. The Executive Secretary,
Tanzania Commission for Universities, P O Box 6562, Dar es Salaam
Tel: +255 22 2772657 and +255 22 2772869; Fax: +255 22 2772891;
Email: dad@tcu.go.tz or admission@tcu.go.tz
Mobile Numbers:+255759 539987, :+255759 537659, :+255714 582742, :+255783
600424 and :+255773 971363
Physical address: Garden Road, Mikocheni, Dar es Salaam
2. The Executive Secretary,
The National Council for Technical Education, P O Box 7109, Dar es Salaam
Tel: +255 22 2780077 and +255 22 2780312; Fax: +255 22 2780060;
Email: es@nacte.go.tz or admissions@nacte.go.tz
Mobile Numbers: +255 767 129132 and +255 767 129134
Physical address: Mikocheni Light Industrial Area, Adjacent to the Institute of Tax
Administration, Dar es Salaam.
-------------------------------------------------------
Baadhi ya mambo muhimu ni haya:
Important dates
| S/N | Activity | Date* |
| 1 |
Lodging of applications for applicants who completed studies between 1988 to 2011 | 1st April |
2
| Lodging of applications for applicants who have completed
studies in 2012 | After the release
of their results |
| 3 | Deadline for submission of applications for all applicants | 30th June |
* NB: An almanac with specific dates will be issued for every admission cycle
Entry routes into higher education institutions
For academic year 2012/2013, applicants into higher education institutions will be categorized
as follows:
a) Direct Applicants include:
i) All who completed their Advanced Level Secondary Education in years
2010, 2011 and 2012;
i i) All who completed their Ordinary Diploma (NTA level 6) in years
2009/2010, 2010/2011 and those who will complete their studies in
2011/2012; and
iii) All who completed their Diploma in Teacher Education in years 2009/2010,
2010/2011 and those who will complete their studies in 2011/2012
b) Indirect Applicants
i) All who completed their Advanced Level Secondary Education in years
1988 to 2009;
ii) All who completed their Ordinary Diploma (NTA level 6) in the year 2008;
and
iii) All who completed their Diploma in Teacher Education in years 1988 to
2009.
c) Equivalent Applicants include holders of:
i) Diplomas (Non-NTA level 6) offered by Tanzanian institutions and have been
recognized by NACTE;
ii) Diplomas from outside Tanzania which have been recognized by NACTE;
iii) Bachelor degrees related to the sought programme. e.g. B.Com --aB.A
Economics;
iv) Post-Form VI Certificates of one year and above offered by universities or
professional bodies such as NBAA and PSPTB (former NBMM) that have been
recognized by NACTE.
NB: 1. All applicants under Category a) and b) will apply through the Central
Admission System
2. All applicants under Category c) will apply directly to institutions of
their choice.
------------------------------------------------------------------------------------------------
Kwa maelezo zaidi, namna ya ku-apply na mambo mengine muhimu tembelea website ya TCU,
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), jana kilikuwa katika furaha baada ya Mbunge wake wa Ubungo, John Mnyika kuthibitishwa na Mahakama Kuu kuwa Mbunge halali wa Ubungo jijini Dar es Salaam.
Ubunge wa Mnyika ulikuwa unapingwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam na aliyekuwa mgombea wa CCM, Hawa Ng’humbi.
Mahakama hiyo jana kupitia kwa Jaji Upendo Msuya, ilitamka kuwa uchaguzi katika jimbo hilo ulikuwa wa halali na kura alizopata Mnyika ni halali.
Aidha, Jaji Msuya alisema maombi ya Ng’humbi kuwa mahakama hiyo ibatilishe matokeo yaliyompa ushindi Mnyika yametupwa kwa kuwa hakuthibitisha madai yake na kutakiwa kulipa gharama za kesi hiyo aliyoifungua mwaka 2010, siku chache baada ya kubwagwa na kijana huyo.
Awali kabla ya kusomwa kwa hukumu hiyo, Mahakama hiyo jana ilijaa wanachama na wapenzi wa Chadema na CCM na kusababisha askari Polisi kufanya kazi ya ziada ya kutanda kila mahali katika mahakama hiyo na katika Barabara ya Kivukoni kuanzia Mahakama ya Rufaa wakiwa na magari ili kuimarisha ulinzi.
Hukumu hiyo ilisomwa na Jaji Msuya mahakamani hapo kwa takribani saa moja na nusu kuanzia saa 4 asubuhi ambapo pia amuru gharama za kesi hiyo kubebwa na Ng’humbi ambaye kabla ya kuwania ubunge mwaka 2010, alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma.
Jaji Msuya alisema Ng’humbi katika madai yake yote matano hakuna hata moja alilolithibitisha kama ambavyo sheria inamtaka mdai katika kesi ya uchaguzi, kuthibitisha dai lake bila kuacha shaka yoyote na kutoa ushahidi kuonesha ni namna gani iliathiri matokeo ya uchaguzi.
Alisema Ng’humbi na mashahidi wake aliowaita mahakamani, hawakuonesha wala kuthibitisha madai yaliyowasilishwa hapo kwamba yalitendeka na namna gani madai hayo yaliathiri matokeo ya uchaguzi uliofanyika Oktoba 31, mwaka juzi.
“Nilipata nafasi ya kupitia ushahidi wa kila shahidi pamoja na vielelezo vilivyotolewa mahakamani katika kesi hii, lakini nimeshangaa ni kwa nini mdai hakuleta mahakamani mashahidi ambao walikuwepo katika chumba cha majumuisho ya kura ambako ndiko madai hayo yalikotokea,” alisema Jaji Msuya.
Alisema hakuelewa ni kwa nini watu zaidi hawakuletwa kuunganisha ushahidi wao kuthibitisha madai ya mdai na kuhoji kama kweli madai hayo yalitokea, ni kwa nini wagombea wengine au watu waliokuwa katika chumba cha majumuisho hawakulalamika?
Katika madai ya Ng’humbi ya dosari ya kura zaidi ya 14,000 alizodai hazieleweki zimetoka wapi, Jaji alisema alipata nafasi ya kuhesabu kura walizopata wagombea wote wa vyama vilivyogombea jimbo hilo ambavyo ni 16 na kubaini ilikuwa ni kosa tu la kibinadamu na halina uhusiano wowote na mdaiwa wa pili, Mnyika.
Kwa mujibu wa Jaji Msuya, fomu namba 24 b ilikuwa na dosari na ndiyo ilikuwa inabishaniwa na Ng’humbi kwa kuwa ilikosewa kuandika.
Alisema Mnyika alitangazwa kuwa ni mshindi baada ya kupata kura 66,742 wakati Ng’humbi alipata kura 50,544 na wagombea wote kuwa kura 132,496.
Jaji Msuya alisema katika ushahidi wa Ng’humbi, hakuonesha ni vipi ongezeko hilo la kura liliathiri matokeo ya uchaguzi na vipi Mnyika alihusika na ongezeko hilo.
Kabla ya kuanza kuchambua hoja za Ng’humbi, Jaji Msuya aliwapongeza mawakili katika kesi hiyo ambao walijitahidi kuwasilisha mashahidi na kuhoji maswali ya msingi.
Alisema mawakili hao hawakupoteza muda kwa kuuliza maswali yasiyo na msingi wala kuwasilisha pingamizi zinazosababisha shauri kuwa na mlolongo mrefu.
Mnyika aliwakilisha na wakili Edson Mbogoro wakati wakili wa Ng’humbi alikuwa Issa Maige na Mwanasheria Mkuu wa Serikali aliwakilishwa na Justus Mlokozi.
Kuhusu madai ya Ng’humbi kuwa alidhalilishwa kwa kuitwa fisadi na Mnyika katika mkutano alioufanya katika kampeni kwamba aliuza nyumba ya Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania (UWT), na kwamba watu wasichague CCM inakumbatia mafisadi, Jaji Msuya alisema hayakuwa na ushahidi.
Alifafanua kwamba Ng’humbi alidai maneno hayo yalizungumzwa na Mnyika katika mkutano uliokuwa na watu zaidi ya 500, lakini yeye hakuwapo. Kutokana na kukosekana kwa uwepo wake, Jaji Msuya alisema Mahakama haichukui maneno ya kuambiwa, bali mtu aliyesikia mwenyewe au kushuhudia.
“Katika watu wote hao 500 waliokuwa katika mkutano huo, hakuja hata mtu mmoja kutoa ushahidi na pia haikuthibitishwa ni namna gani iliathiri uchaguzi na hivyo hoja hiyo imeondolewa,” alisema Jaji Msuya.
Kuhusu madai kwamba Mnyika aliingia na wafuasi wengine wa Chadema katika kujumlisha matokeo, Jaji Msuya alisema ushahidi pekee ni wa Ng’humbi na kwamba hadhani kuwa ni jambo linalowezekana mtu asiyehusika kuingia katika chumba cha majumuisho ya kura wakati kulikuwa na ulinzi.
Alisema mbali na ulinzi, hata wagombea wengine wangelalamikia jambo hilo, lakini Ng’humbi hakuleta mashahidi waliokuwa katika chumba hicho kutoa ushahidi kuwa kuna watu wasiohusika waliingia.
Kuhusu madai kuwa Msimamizi wa Uchaguzi alitumia kompyuta za mkononi (laptop) za Mnyika badala ya kompyuta rasmi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na pia hazikukaguliwa kiasi cha kutia shaka kuwa pengine kulikuwa na taarifa zisizo rasmi katika kompyuta hizo ikiwa ni pamoja na ongezeko lile la kura 14,000, Jaji Msuya alisema ushahidi umeonesha kuwa kompyuta hizo hazikutumika.
Alifafanua kwamba kompyuta zilizotumika zilikuwa za mawakala na kwamba katika madai hayo, Ng’humbi angeweza kuleta mashahidi zaidi kuthibitisha akiwemo aliyekuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi, Rajab Kiravu.
“Tofauti ya kura kama nilivyosema nimepiga hesabu na nimeona kuwa ni matatizo ya kibinadam na hakuna athari yoyote katika matokeo ya uchaguzi, ni shahidi wa tatu pekee aliyekuja kutolea ushahidi hili na Ng’humbi angeweza kuleta mashahidi zaidi,” alisema Jaji Msuya ambaye alianza kuisikiliza kesi hiyo kuanzia Aprili 19, mwaka huu na majumuisho ya pande zote yalifanywa Mei 4, mwaka huu.
Baada ya hukumu hiyo, Mnyika alikumbatiana na Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe ambaye alikuwapo mahakamani hapo. Pamoja walitoka nje, Mnyika akiwa amebebwa na wafuasi wa Chadema wakiimba na kushangilia kwa ushindi huo.
Hata hivyo, hakukuwa na vurugu kubwa zilizokuwa na madhara zaidi ya maandamano yaliyoondoka mahakamani hapo wakiimba.
Mbowe aliwaeleza waandishi wa habari kuwa kesi hiyo imetumia zaidi ya Sh bilioni mmoja na kutaka kabla ya kusikiliza kesi kama hiyo, uchunguzi ufanyike kwanza ili ikionekana haina hoja za msingi, itupwe mapema.
“Mahakama imetenda haki na hii inaonesha namna ambavyo inaweza kutenda haki hata katika vyama vya upinzani,” alisema Mbowe.
Naye Ng’humbi alisema amepokea uamuzi uliotolewa, lakini hawezi kusema lolote kwa sasa na kuwataka wana CCM wawe na utulivu kwa sababu anaamini ni watulivu na kama kuna jambo tofauti, atazungumza baadaye.
Hadi sasa, Mahakama imekwisha kutengua matokeo ya ubunge ya mwaka 2010 katika majimbo mawili pekee, Arusha Mjini kwa Godbless Lema wa Chadema na Sumbawanga Mjini lililokuwa la Aeshi Hilary wa CCM.
Majimbo ambayo kesi zao zilitupwa na mahakama na wabunge wake kuendelea na nafasi zao ni Segerea, Kasulu Mjini, Biharamulo, Singida Mashariki, Ilemela, Nyamagana, Kilwa Kusini, Muhambwe na Meatu.