Longido
The tour to the extensive plains around longido mountains, 80 km north of Arusha, features an insight into the traditions of Maasai culture. The lush area is home to rare birds and animals.
The tour includes:
- A nature trail to spot birds
- A climb to the impressive Longido mountain through a dense natural forest
- Walking safari through the Maasai plains and over the slopes of Longido mountain
- A visit to a traditional Maasai village
- A tour of historical sites dating back to British colonial times
Tour options:
Half day tour
Full day Tour
A new attraction is a four day trekking trip -from Longido to the Big Rock and Kitumbeine, on to lake Natron.
Longido mountain climb
Day 1
Walk to the campsite of Kimokouwa and go for the full day tour.Day 2
Where to stay
A good number of guest house is currently available within and around the town of Longido. Many more are in pipeline. Camping ground installed with modern toilet facilities is available. Arrangements for camping and hiring equipments and various activities of your interest will be organized by Local Tour Guides or coordination office. An option for staying in a Maasai boma for overnight can be smoothly organized. There are options for several days’ tour in the Maasai land and a long climb of Mount Longido for those doing exercise before trying to conquer the ‘Roof of Africa’ Mount Kilimanjaro. Fly camping will be the best option.
Tour Guides:
The Local Guides are of the Maasai tribe and will guide you well in English and where necessary sign language will be used. They have good experience in guiding tourists in the area and deep cultural insight. Various excursions and tours can be booked through Tanzania Tourist Board-Tourist Information Office in Arusha or through your tour operator/travel agent/lodge & Hotel Operator
Getting there:
Longido is located about 80kms North of Arusha town. Its an hour drive via Arusha Nairobi high way. From the main bus stand in Arusha catch a bus or shared taxi leaving for Namanga and get off at Longido
(Income f rom tourist visits will be used to improve the primary and secondary school classrooms,teachers' houses and water projects.)
For further information contact:
Tell: +255 787 855185 /+255 27 2539209 / +255 715 855185
E-mail: touryman1@yahoo.comThis e-mail address is being protected from spam bots, you need JavaScript enabled to view it
| | |
Mamba / Marangu
Mamba and Marangu in the Kilimanjaro area have both natural and cultural
heritage to offer the visitor. There are more than seven waterfalls in the vicinity,
unique flora with tree, flower and fruit nurseries and fauna. Tour the slopes of
Mt.Kilimanjaro and ascend to beautiful viewpoints.
heritage to offer the visitor. There are more than seven waterfalls in the vicinity,
unique flora with tree, flower and fruit nurseries and fauna. Tour the slopes of
Mt.Kilimanjaro and ascend to beautiful viewpoints.
Tours through Marangu afford panoramic views of
Mt.Kilimanjaro. Visit the home and memorial of the
late Yohana Lauwo, a Marangu native who accompanied
Dr.Hans Meyer on the first recorded climb of Kilimanjaro in 1889,
and read the original log books of Lauwo.
Mt.Kilimanjaro. Visit the home and memorial of the
late Yohana Lauwo, a Marangu native who accompanied
Dr.Hans Meyer on the first recorded climb of Kilimanjaro in 1889,
and read the original log books of Lauwo.
Customised half day, full day or two day walking safaris
can be organised. These tours include the Kinukamori and
Moonjo falls and a visit to a Chagga house made of
straw-roofing . See the first coffee tree planted in
Tanzania and climb up Ngangu Hill. A trip to the African Art Centre
that houses a collection of ancient and modern sculptures, carvings
and paintings is rewarding.
can be organised. These tours include the Kinukamori and
Moonjo falls and a visit to a Chagga house made of
straw-roofing . See the first coffee tree planted in
Tanzania and climb up Ngangu Hill. A trip to the African Art Centre
that houses a collection of ancient and modern sculptures, carvings
and paintings is rewarding.
Mamba is a paradise for bird-watchers and nature lovers. Enjoy scenic
waterfalls, tree, flower and fruit nurseries, pass historical sites the Laka
Holes- large hiding caves used during the Chagga - Maasai wars,
visit a wood carving school, meet a local blacksmith using ethnic methods
to prepare spears and tools, and experience Chagga culture by visiting a
traditional Chagga culture by visiting a traditional chagga house.
waterfalls, tree, flower and fruit nurseries, pass historical sites the Laka
Holes- large hiding caves used during the Chagga - Maasai wars,
visit a wood carving school, meet a local blacksmith using ethnic methods
to prepare spears and tools, and experience Chagga culture by visiting a
traditional Chagga culture by visiting a traditional chagga house.
Tour guides:
The guides of the Cultural Tourism Programme are of the Wachaga tribe who knows well the area, their culture & history and speaks English. Provision of outstanding customer service have been their life long way of life
The guides of the Cultural Tourism Programme are of the Wachaga tribe who knows well the area, their culture & history and speaks English. Provision of outstanding customer service have been their life long way of life
Bookings for various excursions and tours can be made at Tanzania Tourist Board-Tourist Information Office in Arusha or through your tour operators/travel agents/lodge & Hotel Operators
Getting there:
Located at the foot of the’ roof of Africa’ one will catch a bus at Moshi town leaving for Marangu. Its a 45 minutes drive from Moshi town. Local Tour Guides will pick you at the bus stand on arrival. Mamba is located 3 kms from Marangu where walking or riding is possible. For those travelling from Dar-es-salaam will be supposed to get out at Himo Bust stand and then connect with mini-buses to Marangu.
Where to stay:
A wide range of Guest houses, lodges and hotels are available in Marangu and Mamba areas. A number of Homestay houses are available withing and around various villages bordering Kilimanjaro National Park. Camping ground installed with modern toilet facilities and clean water supply is available. Camping gears for hire at reasonable price are available in Moshi town
A wide range of Guest houses, lodges and hotels are available in Marangu and Mamba areas. A number of Homestay houses are available withing and around various villages bordering Kilimanjaro National Park. Camping ground installed with modern toilet facilities and clean water supply is available. Camping gears for hire at reasonable price are available in Moshi town
(Income from tourist visits will be used towards developing educational projects in the Kilimanjaro area)
For further information contact:
Tel: +255 754 818273/ +255 754 038265 / +255 754 390084
email: marvellouscreation@mailcity.comThis e-mail address is being protected from spam bots, you need JavaScript enabled to view it
| |
Mbeya
Mbeya lies about 872 km south-west of Dar es Salaam, its landscape characterized by relief forms created by the volcanic effects of the African Rift Valley.A visit to the region includes:
- A visit to the Ngozi Crater Lake
- A view into the traditional culture of the people of Mbeya
- Climbs to different mountain peaks in the area overlooking the East African Rift Valley
- Visit to the Mbozi Meteorite Stone and the Natural Bridge at Kiwira
Different tours are on offer:
Climb to Mbeya peak
Reaching the Mbeya peak (2,826m) is a steep climb taking about three hours. As you go along the mountain slopes, you see the indigenous flowers and colourful butterflies.
Ngozi Crater Lake
Ngozi Crater Lake lies 38 km south of Mbeya, in the direction of Tukuyu and Lake Malawi. A narrow footpath winds uphill through a dense tropical jungle full of bamboo and wild banana trees. Small mammals and colourful birds hide behind the thick vegetation. After a climb of one hour, you arrive at the crater rim for a magnificent view of the crater lake.
Kiwira Natural Bridge and waterfalls
The Kiwira Bridge was created by the powers of a fast flowing river. Locals call this miracle ' Daraja la Mungu' or ' Bridge of God'. Worth visiting are the nearby Kijungu waterfalls.
Rungwe Mountain climb
Rungwe Mountain at 2,960m is the highest peak in southern Tanzania. This volcano, active over the past million years, dominates the whole area around Tukuyu. It is a vast wild area, more than 100 sq km of forest, upland scrub and rock terrain, completely uninhabited and visited only occasionally. Take a long hike to the crater rim.
Matema beach
The 130 km drive from Mbeya to Matema beach is among the most scenic in Tanzania. A winding road passes through high mountains and tea estates before it descends to the tropical shores of Lake Malawi. From Matema, you can make canoe trips with fishermen over the lake to the nearby village where women specialise in pottery,and to the mouth of the river to spot hippos and crocodiles. It is also possible to organize hikes to the Livingstone Mountains.
Mbozi meteorite and Sisi kwa Sisi farm
40 km south- east of Mbeya, lies the meteorite stone of Mbozi. This is the eighth largest meteorite in the world, weighing about 12 tonnes and dates back to atleast a thousand years. Nearby the stone, the Sisi kwa Sisi society is worth a visit to experience true African rural life.
Other attractions
Several hot water springs, an underground crater known as 'bat caves', ruins of a 200 year old fort, Kaporogwe falls and Usangu basin are some of the other sites.
Where to stay
A wide range of guest houses, hotels and lodges is available in and around Mbeya city. Camping grounds are available in various places including the urbun area, villages and the area near or within Forests of the Southern Highlands at affordable rates. in Mbeya. Camping equipments are available at affordable rates in Mbeya. Coordination office or our local tour guides will assist in making arrangements for home-stay and overnights in the villages, local gu est houses, lodges when making extended tours.
Tour guides
Our local tour guides were born and raised in Mbeya region.This gave then enough time to learn the life of the people, environment the culture & history of the area. They are trained guides who speak good English and will always provide to you an outstanding customer service during your visit.Bookings for various excursions and tours can be made at Tanzania Tourist Board - Tourist Information Centre - Dar es salaam and Arusha or at Mbeya's Cultural Tourism coordination office located at ........ But also you can book through your tour operators/travel agent/ Lodge & Hotel operator
Getting There:
TMbeya is located in Southern highlands of Tanzania, about 10 hours tdrive from Dar es salaam. Daily bus transport is available but atleast one day before booking is appropriate.Train transport services by TAZARA can be another fairly good option. Mbeya is also linked with local charters.
(Income from tourist visits will be invested in agricultural projects of the Sisi kwa Sisi Society)
For furtherinformation contact:
MbeyaTel: +255 754 463471 /+255 754 087689
Email: sisikwasisitours@hotmail.comThis e-mail address is being protected from spam bots, you need JavaScript enabled to view it sisikwasisitours@hotmail.com
| |
llkurot is situated about 20 km west of Arusha town .
The folowing is on offer under this programme:
- A visit to a Maasai boma to see the traditional houses and lifestyle of the Maasai
- A visit to a Maasai holy tree where the Maasai offer sacrifices as part of rituals.
- A traditional Maasai meal prepared by Maasai ladies. Delicacies include "nyama choma" or barbequed meat,green vegetables,herbal tea, coffee, fresh milk, cassava, sweet potato, bread, eggs and fruits.
- A five-day safari, during which you can hire a camel or donkey to view animals -girraffe, zebra, rabbit, hyena, Thomson's gazelle and dik dik- and birds and watch the Maasai graze their cattlein the scenic pastures.
- Watching Maasai dances, groups of artisans and their handcrafts, traditional healers and bee-keepers
- A visit to the Kilimamoto crater, Ngorora hill, waterfalls, valleys and Mt.Meru
- Getting familiar with swahili and Maasai terminology
- Talks with local society members
- A visit to a Maasai women's handicraft group that makes ornaments from beads and natural products.
Tours at Ilkurot can be divided into three excursion categories:
1. Half day walking tour
2. Full day walking tour
3. Three or five day walking safari
The visitor can choose any of the above options
(Note: Those wishing to stay overnight need to bring or hire camping equipment)
Where to stay
Our visitors have a good chance to stay in Arusha town and pay a day visit to our Maasai village locate just 25kms North-West of Arusha along Arusha-Nairobi highway. Camping ground installed with necessary facilities is available. Arrangements for camping and hiring equipments and various activities of your interest will be organized by Local Tour Guides or coordination office. An option for staying in a Maasai boma for overnight can be smoothly organized for you.Tour Guide
The Local Guides are of the Maasai tribe and wears traditional Maasai clothes. Our guides speak English and knows well the Maasai culture.
Arusha or through your tour operator/travel agent/lodge & Hotel Operator
Getting there:
Our visitors can board a minibus (with yellow side line) to Ngaramtoni and then take another minibus going to Oldony sambu where you will get off at Sitau and the sign board will direct you to our office. You can also get other buses going to Namanga (Tanzania-Kenya Border) and get off at Sitau as well. Our guides can pick you at Tanzania Tourist Board –Tourist Information Centre in Arusha town
(Income from tourist visits will be used to support the Ilkurot community and the preservation of the Maasai culture)
For further information contact:
Tel: +255 784 459296/ +255 713 332005 /+255 652 706572
E-mail: kinyorllomon@yahoo.com
Nilifika Wilaya ya Mikindani, mkoani Mtwara kwa mara kwanza miaka kumi na nne iliyopita. Nilipofika Mikindani kwa lengo la kuona majengo ya kihistoria niliona mengine bado yanaweza kukarabatiwa. Katika safari hiyo nililiona boma la Mjerumani, ambalo lilionyesha kuwa ni kivutio kwa watalii wengi, lakini kasoro iliyojitokeza halikuwa likitunzwa vizuri sana.Lakini ukienda leo hali ya jengo hilo siyo ile niliyoiona awali. Jengo limechukuliwa na wazungu walioligeuza kuwa hoteli. Kwa kweli linatunzwa vizuri sana. Na kilichofanyika ni kujitahidi kulirudishia kama lilivyokuwa awali. Linavutia na kwa kweli sio tena lile jingo chafu la Boma la Mjerumani kama unavyoyaona mengine ambayo hayatunzwi katika maeneo mbalimbali nchini. Kutokana na hali hiyo nilijiuliza kwamba tunataka kutunza majengo yetu ya historia kwa kusubiri ufadhili kutoka nje tu! Jambo la ajabu zaidi, Serikali imekuwa ikiwapa wananchi majengo ya kihistoria amabayo wanayabomoa na kujenga ujenzi wanaoutaka. Historia inafutwa, kumbukumbu zinafutwa, na hakuna anayejali. Tumekaa tu!. Serikali inazungumzia kuhifadhi na kukuza vivutia vya utalii. Ni utalii upi? Inasema kuwa inataka kuhimiza utalii wa ndani. Ni utalii upi? Kama hata vivutio vilivyoko karibu na wananchi havitunzwi, tutawasaidia vipi watalii (wananchi) wa ndani ambao wamekuwa wakishindwa kutembelea mbuga zetu na vivuti vingine? Tunapowaachia wageni uwezekano wa wananchi kufika katika majengo ya kihistoria ambayo yamegeuzwa kuwa hoteli ni mdogo kwa kuwa watahofia kuwapo kwa gharama kubwa za kuingia hapo. Nilifika Unguja na kutembelea makazi ya Sultan Seyd Barghash kuna makazi yaliyodumu kwa miaka zaidi ya mia sasa. Kuna miembe mingi yenye umri mkubwa sana tangu yalipopandwa na sultani huyo. Nilidhani Serikali ingetafuta fedha na kuboresha bustani ya Unguja na kukarabati jengo la Barghash na kuweka huduma za buradani. Watalii na wananchi, na hasa wanafunzi, wangeweza kufika hapo na kujifunza mengi kuhusu historia ya taifa hili. Lakini jengo lile la Barghash linapotea na kuharibika kadri siku zinavyokwenda. Kutokana na hali hiyo miaka 10 ijayo jingo hilo halitakuwapo. Nilifika Ras Mkambuu Pemba ambako kuna historia ya taifa tangu miaka mingi tangu Kuzaliwa kwa Yesu Kristo, historia inayotuunganisha na Wairan,(Washiraz kutoka Iran kusini), lakini majengo, makaburi, misikiti na visima vinapotea na siyo muda mrefu vitamezwa na maji ya bahari. Hakuna mtu anayejali. Wahifadhi watakuambia wanahangaika kutafuta wafadhili kutoka nje ili wawasaidie kutunza historia ya Tanzania. Kweli wageni wanakusaidia kutunza historia ya Taifa! Kutokana na hali hiyo tutaandika katika vitabu vyetu vya historia kuwa majengo hayo yalijengwa na wageni, na yakaokolewa na wageni. Kila jengo limeokolewa na wageni. Historia ikiandikwa na wageni maana yake ni kwamba hatujui tunakotoka na wapi tunakokwenda. source: mwnanchi.co.tz |
Nahodha huyo msaidizi wa Stars, Morris ataikosa mechi hiyo ya Jumapili kwa sababu anatumikia adhabu yake ya kadi nyekundu baada ya kupata kadi mbili za njano katika mchezo dhidi ya Ivory Coast wiki iliyopita ambao pia ulikuwa wa kusaka tiketi ya kushiriki fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika Brazil 2014. Kim alisema hayo jijini Dar es Salaam baada ya kumalizika kwa mazoezi ya jana asubuhi ya kikosi hicho kwenye Uwanja wa Karume. “Aggrey (Morris) hatakuwepo kwenye mchezo wa Gambia, anatumikia adhabu ya kadi nyekundu aliyopewa Ivory Coast, lakini nitamwanzisha Nyoni kucheza nafasi yake,” alisema Kim. “Nilimwona anavyocheza dakika chache kwenye mchezo wa Ivory Coast, alicheza vizuri na kwa utulivu, ni mchezaji mzoefu na anajua jinsi ya kumdhibiti adui.” Alisema, "hakuna mabadiliko makubwa kwenye kikosi, nafikiri hakutakuwapo na sura mpya zaidi ya wale waliocheza mchezo uliopita na Ivory Coast." "Nafikiri itawasaidia kuelewana na kucheza kwa mpangilio ulio sahihi, nafahamu kila mmoja wetu anataka kuona tunaifunga Gambia," alisema Kim. Aliongeza kuwa hana wasiwasi kukosena kwa Morris kwani anawaamini wachezaji wote aliowaita kwenye kikosi hicho kwamba ni wazuri na wenye kucheza nafasi zaidi ya moja uwanjani. “Kila namba nilijaribu kuita wachezaji wawili, nilifahamu inaweza kutokea mmoja ameumia au kutumikia adhabu ya kadi, nafikiri yote yametukuta, lakini tunasonga mbele," alisisitiza Kim. Kocha huyo amemwondoa kwenye kikosi hicho beki wa Simba, Masoud Nassoro 'Chollo' kutokana na kuumia goti. Daktari wa timu hiyo Mwanandi Mwankemwa alisema, "uchunguzi unaonyesha tatizo hilo ni la muda mrefu kwa Chollo, alijitonyesha, atachukua muda kidogo kurudi katika hali yake ya kawaida." Wachezaji wengine ambao walikuwa majeruhi, lakini wamejiunga na wenzao na kufanya mazoezi ni viungo, Haruna Moshi 'Boban' na Nurdin Bakari. Wakati huohuo; mtaalamu wa tiba ya viungo wa klabu ya Azam FC, Paulo Gomez amejitolea kuwafanyisha mazoezi maalumu Haruna Boban' na Nurdin ili warejee kwenye kikosi cha Stars haraka. Boban, Bakari, Said Nassoro 'Cholo'na Thomas Ulimwengu hawakujumuishwa kwenye kikosi cha Taifa Stars kilichoikabili Ivory Coast ugenini kutokana na kusumbuliwa na majeruhi. Mmoja wa viongozi wa bechi la ufundi la Taifa Stars aliliambia Mwananchi kuwa Gomez pia ndiye alichunguza afya za wachezaji wote wa timu hiyo siku mmoja kabla ya safari ya Ivory Coast na kubaini matatizo kwa Boban na Cholo yaliyosababisha kuondolewa kwao. Akizungumza na Mwananchi mara baada ya kumaliza programu yake ya mazoezi na wachezaji hao kwenye Uwanja wa Karume, Gomez alisema anafanya kazi hiyo bila malipo yoyote kutokana na mapenzi yake kwa Tanzania. "Mimi ni mtaalamu wa tiba za viungo, TFF iliniomba nije niwasaidie na mimi nilikubali kwa moyo mmoja. "Hapa nilipo najitolea tu silipwi chochote na mimi naridhika kwa sababu napenda kuisaidia Tanzania,"alisema Gomez. Gomez alisema kuwa mazoezi anayowapa Boban na Bakar yana lengo ya kumaliza maumivu na kuwarejesha katika hali ya kawaida. "Mazoezi haya yanachukua dakika 45 mpaka saa moja, ni aina ya mazoezi ambayo lengo lake ni kumwezesha majeruhi kurejea katika hali ya kawaida,"alisema Gomez. source: mwananchi.co.tz |
ASEMA WANAOUNUNG’UNIKA WAKO HURU KUJIONDOKA
SIKU nne baada ya kung’olewa aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Paul Chizi, Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe ameamua kuanika tuhuma za ufisadi zinazodaiwa kufanywa na kigogo huyo.Miongoni mwa tuhuma hizo ni kuingia mkataba wa kununua ndege bila kumhusisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali(AG) na kununua sare 15 za watumishi wa ndege kwa dola 50,000 za Marekani.
Juni 5, Dk Mwakyembe alitengua uteuzi wa Chizi na kumteua rubani wa muda mrefu, Kapteni Lusajo Lazaro kukaimu nafasi hiyo, akisema uteuzi ulikiuka Sheria za Utumishi wa Umma.
Mbali na kutengua uteuzi huo, pia alitangaza kuwasimamisha kazi vigogo wengine wanne wa shirika hilo, hatua ambayo ilianza kuibua malalamiko kutoka kwa baadhi ya wafanyakazi kwamba hatua hiyo ilitokana na majungu na ukabila.
Waliosimamishwa kazi na Dk Mwakyembe ni Kaimu Mkurungenzi wa Uhandisi, Jonh Ringo, Mwanasheria ,Amini Mziray, Kaimu Mkurugenzi wa Fedha, Justus Bashara na Josephat Kagirwa ambaye alikuwa Kaimu Mkurugenzi wa Biashara.
Jana, waziri huyo wa uchukuzi aliamua kufafanua tuhuma moja hadi nyingine zinazomhusu kigogo huyo na wenzake na kusema, mbali ya tuhuma za Chizi, wakurugenzi wawili wa shirika hilo walikwenda kushonesha sare 15 za wahudumu wa ndege nchini China kwa gharama ya dola 50,000 za Marekani (karibu Sh80 milioni).
Akizungumza na wafanyakazi wa shirika hilo katika Uwanja wa Ndege wa zamani (Terminal One) jijini Dar es Salaam, Dk Mwakyembe alisema kutokana na hali hiyo, ameagiza kujazwa kwa nafasi zilizo wazi na kuwaonya watakaozichukua, kuhakikisha wanachapa kazi ili ATCL ipige hatua na kama wakishindwa watakuwa wamejiondoa wenyewe.
Dk Mwakyembe alitoa miezi mitatu kwa shirika hilo kuanza kujiendesha kwa faida, ikiwa ni pamoja na kupata fedha za kuwalipa wafanyakazi wake.
“Kwa kasi niliyoanza nayo watu kama Chizi ni lazima wakae pembeni, ni mtaalam katika masuala haya, lakini tatizo lake hakuwa muwazi,” alisema Dk Mwakyembe.Chizi hakupatikana jana kuzungumzia tuhuma hizo, wakati wote Mwananchi ilipompigia simu yake ya kiganjani, ilikuwa imezimwa.
Waziri huyo ambaye pia ni Mbunge wa Kyela, alitumia Saa 1:17 kuzungumza na wafanyakazi hao na kufafanua kwamba Serikali imechoka kutoa fedha za kuliendesha shirika hilo, akihoji iweje mashirika mengine ya ndege yaweze kusimama yenyewe, lakini ATCL iishindwe.
“Tunaipenda ATCL iendelee na tunachukua hatua za kila aina ila tukiona tunashindwa tutaachana nalo ili, fedha zinazotumika hivi sasa zipelekwe kufanyia mambo mengine ya maendeleo,” alisema Dk Mwakyembe.
Tuhuma
Akichambua tuhuma moja hadi nyingine za ukiukwaji wa sheria na taratibu, Dk Mwakyembe alianza kwa kutolea mfano mkataba tata baina ya shirika hilo na Air Bus ambao umeifanya nchi kudaiwa Sh69 bilioni na kusisitiza kuwa, kutokana na hali hiyo Serikali haikuwa tayari kufumbia macho mambo mengine ya ovyo yaendelea katika shirika hilo.
Alisema wafanyakazi wote wa ATCL ambao wananung’unika baada ya kutengua uteuzi wa Chizi wako huru kuondoka katika shirika hilo, huku akionya atawatimua wengi watakaofanya mambo kinyume.
“Nilipoteuliwa kuwa waziri wa uchukuzi siku chache baadaye nilisikia ATCL wanaleta ndege mpya, nilimwita Katibu Mkuu wa wizara anipe ufafanuzi wa jambo hilo, lakini, akaniambia hafahamu lolote,” alisema Dk Mwakyembe.
Aliongeza, “Ndege hiyo ilikodishwa na kutua nchini kwa mara ya kwanza mwezi uliopita kutokana na iliyokuwapo kuanguka mkoani Kigoma. Ndege hiyo aina ya Boeing 737-500 imekodishwa kutoka Kampuni ya Aero Vista ya Dubai.”
Dk Mwakyembe kwa sauti ya ukali alisema, “Niliamua kuwaita wakurugenzi wa ATCL ofisini kwangu saa 3 asubuhi, lakini wakaja saa nne na nusu, pamoja na hayo walinieleza kuwa jambo hilo liko safi na limeshafika kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.”
Alisema baada ya siku moja, alipata taarifa kutoka ofisi ya AG ikieleza kwamba hawana mkataba huo.
“Nikaona jambo zito kidogo, nikaamua kukutana na wale wawekezaji ambao walinionyesha mkataba ule ambao ulipitishwa bila wizara kujua, jambo hilo nililihoji pia…, nawambia ukweli mkataba huu niliuona upande wa pili sio kwa viongozi wa shirika,” alisema Dk Mwakyembe.
Alisema hivi sasa mchakato wa kuchunguza mikataba hiyo umeshaanza na kusisitiza kuwa, hiyo ndio ilikuwa moja ya sababu ya kumng’oa Chizi.
Dk Mwakyembe alisema, “nchi haiwezi kuendelea kwa kukiukwa kwa sheria za ununuzi na ajira. Hata Kapteni Lazaro naye ameponea chupu chupu maana kabla ya kuwang’oa wakurugenzi tulipitia mafaili yao.”
“Msitegemee kubebwa ndugu zangu, nawaomba mchape kazi, mishahara yenu sio mizuri, lakini mkiweza kusimama mtakuwa na uwezo wa kujipangia hata mishahara,” alisema Dk Mwakyembe.
Alisema kwa kutambua mchango wa ATCL, Serikali imepata Sh4.9 bilioni kwa ajili ya matengenezo ya ndege ya shirika hilo na kuwataka kuzitumia kwa ufanisi fedha za shirika hilo.“Hivi sasa inatakiwa kila baada ya miezi mitatu tunakutana na kuzungumza,” alisema Dk Mwakyembe.
Kapteni Lazaro aahidi ushirikiano
Kwa upande wake, Kapteni Lazaro aliahidi kuyazingatia yote yaliyozungumzwa na waziri huyo, huku akiomba shirika hilo kuongezewa muda zaidi kwa kuwa miezi mitatu ni michache ili liweze kujitegemea.
Kupanda/kushuka ATCL
ATCL ni kampuni iliyoanzishwa baada ya Shirika la Ndege la Tanzania ATC kuingia ubia na Shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA) mnamo mwaka 2002.
ATCl ni moja ya mashirika ya ndege yaliyoonyesha kukua kwa kasi miaka ya 1980 na 1990, lakini lilianza kuyumba kutokana na uendeshaji mbovu na hali ikawa mbaya zaidi baada ya kuingia ubia na SAA.
Serikali iliingia mkataba wa ubia na SAA mwaka 2002 kwa matumaini kwamba itakua na kuwa moja ya mashirika makubwa ya ndege Afrika, lakini hali ikawa kinyume chake.
Kwenye mkataba huo, Serikali ikibakia na hisa 49 huku SAA ikiwa nazo 51, ambazo zilimfanya mbia huyo kuwa na nguvu ya kuamua mambo mengi.
Serikali ilivunja mkataba na SAA Septemba 2006, baada ya kubaini kuwa ATCL inazidi kudidimia kiuchumi huku madeni yakiwa yanaongezeka kadri muda ulivyokuwa unaenda
source:mwananchi.co.tz/habari
Waziri kivuli wa Fedha na Uchumi, Zitto Kabwe akitoa taarifa ya vipaumbele vya Kambi ya Upinzani Bungeni katika bajeti ya mwaka wa fedha 2012/2013.
KAMBI ya Upinzani Bungeni imetangaza Bajeti mbadala kwa mwaka wa fedha 2012/13 yenye vipaumbele 10, kikiwamo kinachoitaka Serikali kuhakikisha inapunguza misamaha ya kodi hadi asilimia moja.Pia kambi hiyo imeainisha namna ya kukabiliana na mfumuko wa bei kwa kuhakikisha inawekeza zaidi katika chakula na nishati, ambapo kwa upande wa chakula iruhusu mchele kuingizwa nchini bila kodi ili kupunguza gharama za maisha kwa wananchi.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Waziri Kivuli wa Fedha, Kabwe Zitto, alisema kambi hiyo imebaini kuwa kiwango kikubwa cha misamaha ya kodi cha asilimia tatu kinaweza kupunguzwa, kama nchi nyingine duniani zinavyofanya na fedha hizo kuingizwa kwenye Bajeti ya Taifa.Kambi hiyo inataka maelezo ya kina ya sababu ya Serikali hadi sasa kushindwa kutekeleza ahadi yake iliyoitoa bungeni kuwa misamaha ya kodi itapunguzwa hadi asilimia moja ya Pato la Taifa.
Pamoja na hayo, alisema kambi hiyo imepanga kukabiliana kikamilifu na mfumuko wa bei ambao uko juu, kutokana na kupanda kwa bei za vyakula ambapo, itahakikisha inapunguza kodi kwenye bidhaa za mafuta ya petroli na dizeli.
Vipaumbele hivyo ni:
- Kuhakikisha fedha nyingi zinaelekezwa katika rasilimali fedha kwenye maendeleo vijijini, hasa kujenga miundombinu ya barabara za vijijini, hatua itakayosaidia wakulima kuuza bidhaa zao kwa bei ya chini jambo linaloweza kupunguza umasikini.
- Kusimamia wigo wa kutoza tozo la ujuzi (SDL) ambapo sasa waajiri wanalipa asilimia sita ikiwamo Serikali na mashirika ya umma.
- Kushusha kima cha chini cha Kodi ya Mapato (PAYE) hadi asilimia tisa ili kuwawezesha wafanyakazi wa kima cha chini kumudu maisha hasa mfumuko wa bei.
- Kuongeza mapato ya ndani na kupunguza mikopo ya kibiashara. Alisema katika eneo la mapato ya ndani, kambi hiyo inataka yafikie asilimia 20 ya Pato la Taifa pamoja na kuongeza nguvu za kisheria na udhibiti ili Mamlaka ya Mapato (TRA) ikusanye zaidi kwenye kampuni za simu na katika shughuli za uchimbaji wa madini, mafuta na gesi.
- Kupunguza na kufuta kodi kwenye bidhaa za vyakula kwa muda maalumu, ili kushusha mfumuko wa bei kwani sasa ni asilimia 26 hivyo ni muhimu Serikali ikaruhusu wafanyabiashara wakaagiza mchele kutoka nje kwa miezi mitatu.
- Kuweka mfumo mpya wa elimu kwa kushirikisha sekta binafsi kutoa elimu bora zaidi ikiwamo kuundwa kwa chombo cha udhibiti wa sekta hiyo. Alimpongeza Waziri wa Fedha, Dk William Mgimwa, kwamba amekuwa akionesha uungwana na usikivu na kumtaka apokee maoni ya Kambi ya Upinzani si kwa maslahi ya upinzani, bali kwa manufaa ya Watanzania.
Mwelekeo wa bajeti hiyo ya upinzani unakuja wakati Serikali imeshatoa mwelekeo na vipaumbele vyake mwishoni mwa wiki iliyopita, ambapo inatarajia kutumia Sh trilioni 15; matumizi ya kawaida yakiwa Sh trilioni 10 na maendeleo ni Sh trilioni tano. Kwa mujibu wa Dk Mgimwa, vipaumbele vya bajeti hiyo ni miundombinu ambayo imegawanywa katika makundi ya reli, umeme, maji salama, usafirishaji na uchukuzi ambavyo vimetengewa Sh trilioni 4.5 na vingine ni kilimo, viwanda, rasilimali watu, huduma za jamii, utalii, biashara ya ndani na nje na huduma za fedha
Meneja Mawasiliano wa kampuni ya ya Serengeti Imani Lwinga akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa City Sports Lounge jijini Dar es salaam wakati alipotangaza zawadi kwa washindi wa tuzo za mwanamichezo bora zinazoandaliwa na chama cha waandishi wa habari za michezo TASWA, kulia ni Amir Mhando Katibu mkuu wa TASWA na katikati ni Juma Pinto Mwenyekiti wa TASWA.
(TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI)
MWANAMICHEZO Bora wa Tanzania kwa mwaka 2011 anatarajiwa kupewa dola za Marekani 8,000 (Zaidi ya sh. Milioni 12 za Tanzania).Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, Meneja Mawasiliano wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL), Imani Lwinga alisema uamuzi wa kutoa fedha una lengo la kumpa uhuru mshindi aweze kufanya mambo anayoyapenda kutokana na zawadi hiyo.
“Nia ya kutoa zawadi ni kumfanya mshindi aone ana kitu fulani amepata, hivyo safari hii tumeona tutoe kiasi hicho cha fedha ambacho tunaamini kitakuwa changamoto kubwa kwa mshindi,” alisema Lwinga.Alieleza kuwa walipokea ombi kutoka Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), ambacho ndiyo kinaandaa tuzo hiyo, kwamba safari hii kuwe na mabadiliko kwa mshindi akabidhiwe fedha badala ya zawadi ya gari kama ilivyokuwa mwaka jana. Pia mshindi huyo wa jumla atapewa cheti na kombe.
Lwinga alisema pia Serengti itatoa zawadi ya Sh. Milioni moja kwa kila mshindi wa michezo mbalimbali ambayo itazawadiwa katika sherehe hizo zitakazofanyika Juni 14 mwaka huu ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam.
Akizungumzia hilo, Katibu Mkuu wa TASWA, Amir Mhando alisema wanatarajia wanamichezo mbalimbali watapewa tuzo siku hiyo na kutaja michezo ambayo itapewa tuzo kuwa ni riadha, wavu,netiboli,kuogelea, tenisi, judo, kikapu, soka, ngumi za kulipwa, ngumi za ridhaa, gofu wa ridhaa, gofu wa kulipwa, baiskeli, kriketi.
Mingine ni mpira wa mikono, olimpiki maalum, Mchezaji Bora wa Nje anayecheza Tanzania, Mchezaji Bora Chipukizi, Mchezaji Bora wa Tanzania anayecheza Nje, Karate, Mwanamichezo Bora wa Tanzania mwaka 2011 na Tuzo ya Heshima.
Mhando ambaye pia ni Katibu wa Kamati ya Tuzo alisema Ijumaa watatangaza majina ya wanamichezo wote watakaowania tuzo hiyo na kuipongeza Serengeti kwa udhamini wao wa kila mwaka.
Kwa mujibu wa Mhando mwaka 2006 Mwanamichezo Bora wa Tanzania alikuwa Samson Ramadhan aliyezawadiwa sh. 500,000, wakati mwaka uliofuata mshindi ambaye alikuwa Martine Sulle alizawadiwa Sh.500,000, huku mwaka 2008 mshindi akiwa Mary Naali alizawadiwa sh.750,000. Wote hao ni wanariadha.
Mshindi wa mwaka 2009 alikuwa mchezaji netiboli Mwanaid Hassan aliyezawadiwa sh. Milioni moja na mwaka 2010 pia alikuwa Mwanaid aliyezawadiwa gari aina ya Toyota Cresta GX 100 .
Akizungumza kwenye mkutano huo, Mwenyekiti wa TASWA, Juma Pinto aliwashukuru Serengeti na kusema kuwa ana matumaini zawadi hizo itakuwa kichocheo cha wanamichezo kufanya vizuri zaidi.
Mratibu wa Shindano la Miss Dar Intercollege 2012, Dina Ismail akiwanadi warembo watakaoshiriki shindano la Miss Dar Intercollege 2012 wakati wa uzinduzi wa bendi ya SkyLight ndani ya Mafian Lounge jijini Dar es Salaam wikendi iliyopita.
Warembo wakionesha umahiri wao wa kupita jukwani.
Warembo wakionesha umahiri wao wa kupita jukwani.
Wakipita wa mwendo wa twiga.
Wakifunguliwa shampeni kwa nderemo na vifijo.
Baadhi ya Warembo wa Miss Dar InterCollege wakiwamejipanga mbele ya wadau na wadhamini katika uzinduzi wa bendi ya SkyLight iliyofanyika Mafian Lounge iliyopo Masaki, bendi hiyo inamilikiwa na mmoja wa wadhamini wao Ndege Insurance.
Mratibu wa Shindano hilo Dina Ismail alisema kwamba warembo watakaoshiriki shindano hilo wanaendeleza na mazoezi kwenye hoteli ya Lamada jijini Dar es Salaam chini ya ukufunzi wa Marylidya Boniface, huku kwa upande wa shoo wakinolewa na Bob Rich.
Alisema mpaka sasa warembo 15 kutoka vyuo vya Biashara (CBE), Uandishi wa Habari (DSJ) na Time, Ustawi wa Jamii na kile cha Usimamizi wa Fedha (IFM) wamesharipoti kambini.Dina aliwataja warembo hao kuwa ni pamoja na Hilda Edward, Nancy Maganga, Saada Seleman, Neema Nashon, Rose Muchunguzi, Fina Revocatus, Jane Augustino,Theresia Issaya na Natasha Deo.Taji la kitongoji hicho linashikiliwa na Rose Msuya kutoka IFM.
Kwa upande mwingine, mratibu huyo ameyaomba makampuni mbalimbali kujitokeza kudhamini shindano hilo ambalo linatarajiwa kuwa la aina yake na hasa ikizingatiwa kuwa washiriki wake wana vigezo vya hali ya juu.
“Tunaomba makampuni mbalimbali yajitokeze kudhamini shindano letu…mpaka sasa wadhamini tulionao ni pamoja na kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia ya Redd’s, Lamada Hotel, Ndege Insurance, Dodoma Wine na Clouds Fm.

Diamond mapema leo akiwa katika studio za Clouds FM kwa ajili ya interview.
---
Kwenye kipindi cha XXL leo kinacho rushwa na Clouds Fm msanii Diamond aliulizwa ni kwa vipi aliweza kujielezea vizuri sana kwa lugha ya Kingereza baada ya performance yake kwenye Big Brother StarGame maana wengi huwa wanashindwa ifikapo hatua hiyo Diamond alifunguka na kukiri kwamba mrembo Wema Sepetu amechangia kiasi kikubwa kwake kujua lugha hiyo na kusema napenda kumshukuru 'WEMA ENGLISH COURSE'...... kusema ukweli nilifurahi sana kusikia hivyo maana pamoja na mascandal yao yote angalau Diamond ameweza kuongelea upande mzuri wa Wema na ni jinisi gani ameweza kuchangia mafanikio yake kwa kiasi flani.
Wakati huo huo Diamond pia ameongela tour yake ambayo anatarajia kuifanya nchini Marekani baadae mwaka huu na nyumba anyo jenga Tegeta ambayo amekiri mpaka sasa ametumia karibia Tshs milioni 69. Nyumba ni ya kisasa, ina vyumba vya kulala vinne, vitatu vyote master, kuna studio, jiko, choo, bafu nk. Pamoja na nyumba hiyo kuna zingine pia ambazo hakupenda kuongelea ila I hope and I'm sure kuna siku atafunguka.
Tunapenda kumtakia kila la kheri Diamond na Big Up to mrembo Wema Sepetu kwa msaada alio mpatia Diamond kwa kumfundisha Kingereza.
BAADHI YA WANANCHI WAKISHANGAA BAADA YA FAINES KUZINDULIWA NA MTOTO MWENYE MIAKA KUMI ALIYEKABIDHIWA MIKOBA NA MAMA YAKE
FAINES AKIPAKIWA KATIKA GARI YA POLISI
FAINES ZAWADI-BINTI ALIYEFARIKI KWA MUDA NA KUREJESHWA DUNIANI AKIWA AMESHIKILIWA NA NDUGU ZAKE

MJUKUU BATROMEO BRUNO NA BIBI YAKE EVANIA SEPHANGA WAKISHUKA KATIKA GARI LA POLISI BAADA YA KUFIKISHWA KITUO CHA POLISI CHA KATI CHA KIGOMA
Na Pardon Mbwate na
Felister Chubwa, wa Polisi Kigoma
Jeshi la Polisi mkoani Kigoma limefanikiwa kuwaokoa watu watatu waliokuwa wamezingirwa na kundi la wananchi wakitaka kuwaua kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya ushirikina.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani Kigoma SSP Joseph Konyo, aliwataja watu hao waliokolewa kuwa ni Evania Sephanga(50), mkazi wa wilaya ya Kibondo, Bruno January(46), mkazi wa kijiji cha Nyamhoza na mtoto mmoja mwenye umri wa miaka kumi na mkazi wa kijiji cha Nyamhoza Kigoma mjini ambaye jina lake linahifadhiwa.
Kamanda Konyo amesema kuwa wiki iliyopita majira ya saa tisa mchana, watu hao walizingirwa na kundi hilo kwa madai kuwa walimroga na kumuua msichana mmoja aitwaye Faines Zawadi(20) mkazi wa kijiji hicho cha Nyamhoza ambaye siku moja kabla ya kifo chake alionekana kama mtu aliyechanganyikiwa na kuwa kama kichaa.
Alisema katika tukio hilo, bibi kizee mmoja ambaye alikuwa mshirika wa kundi la waliodaiwa kuwa wachawi, alifanikiwa kutoroka katika mazingira ya kutatanisha alipojifanya kuwa anakwenda kujisaidia.
Kamanda Konyo amemtaja bibi huyo aliyefanikiwa kutoroka kuwa ni Bibi Editha Dosiyo mkazi wa kijiji hicho ambaye baadaye alipatikana na kuhojiwa kabla ya kukabidhiwa kwa Idara ya ustawi wa jamii baada ya kuonekana kuwa maisha yake yangekuwa hatarini.
Amesema baada ya Polisi kupata taarifa za tukio hilo, walikimbia na kwenda kuwaokoa kutoka katika mikono ya kundi la wananchi lakini wakiwa wameshaadhibiwa kwa kupigwa kiasi.
Habari zinasema kuwa, baadhi ya wananchi walipata taarifa kutoka kwa mtoto aliyeokolewa akisema kuwa baadhi ya watoto waliofariki kijijini hapo, akiwataja (majina tunayahifadhi) alikuwa akiwaona nyumbani kwao nyakati za usiku wakiosha vyombo na baadaye kupewa chakula.
Siku ya tukio hilo, baadhi ya wananchi walisema kuwa kabla ya bibi huyo kutoweka alimnong’oneza jambo mjukuu wake ili amfanyie marehemu ikiwa ni pamoja na kumruka mara saba kisha bibi huyo alitoweka akijifanya anakwenda kujisaidia.
Walisema mara baada ya bibi huyo kutoweka, mtoto huyo wa kiume ambaye ni miongoni mwa waliozingirwa wakitaka kuuawa, alianza kutekeleza maagizo ya bibi huyo na alipomaliza kitendo cha kumruka kwa mara ya saba, msichana yuyo ambaye alikuwa 'mfu' alizinduka na kuomba uji.
Wamesema msichana huyo alipewa uji na kunywa kisha akapelekwa hospitalini ambako hadi sasa hali yake inasemekana kuwa inaendelea vizuri.
Hata hivyo Kamanda Konyo ametoa wito kwa wananchi kuacha kuchukua sheria mkononi na badala yake watoe taarifa Polisi kwa kila jambo wanaloliona kuwa linaweza kuleta uvunjifu wa amani ili hatua za haraka zichukuliwe dhidi ya wahusika.
Mwezi uliopita watu wawili mke na mume, waliuawa na kundi la watu wenye hasira kisha miili yao kuchomwa kwa moto mkoani Kigoma baada wa kutuhumiwa kuwa walikuwa ni wachawi.
Baaada ya kazi kubwa ya kuzindua na kuimarisha tawi la chadema Washington Dc Maryland na Virginia,Wabunge wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)Mhe. Peter Msigwa na Mhe. Nassari Joshua, Al-Marufu Dogo janja, Usiku wa Jana Jumatano Mei 30,2011 waagwa rasmi kwa kuangalia mpambano wa kimataifa kati ya US na Brazil ndani ya uwanja wa Fedex, uliopo Landover Maryland Nchini marekani
Wabunge wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mhe, Peter Msigwa na Mhe. Nassari Joshua, Al-Marufu Dogo janja, wakiwa na uwongozi wa tawi la Chadema Washington Dc Libe Mwangombe, wanne, Mjomba a.k.a Cosmas, Mzee wa swahilivilla Aboh Shatry wa pili kulia, pamoja na mashabiki wa US, wakiiunga mkono bendera ya taifa.
(Picha maelezo na swahilivilla.blog spot.com)
Idadi ya wapenzi waliohudhuria katika mpambano huo ni 67,656 wakiwemo Mhe. Nassari Joshua pamoja na Mhe, Peter Msigwa.
Wabunge wa chama cha Chadema wakipata flash ya pamoja na warembo wa Kibrazil ndani ya uwanja wa FedexField, uliopo Landover Maryland Nchini marekani.
Picha ya pamoja na viongozi wa juu wa Chadema kwenye mpambano wa US na Brazil Usiku wa kuamkia leo Alhamis Mei 31,2012 ndani ya ndani ya uwanja wa Fedex, uliopo Landover Maryland Nchini marekani
![]() |
| Forward wa United States Landon Donovan, akipandisha majeshi juu huku alidhibitiwa na Brazil defender Marcelo wa Brazi katika mpambano wa kirafiki. |
Nabendera ya Taifa wakishangilia Bao la kwanza la Brazil lilifungwa kwa Penalti na mchezaji Neymar
