• HOME
  • NEWS
  • ABOUT US
  • ZONAL ATTRACTIONS
    • Lake Zone
    • Southern Zone
    • Eastern & Coastal Zones
    • Central Zone
    • Northern Zone
  • CULTURAL TOURISM PROGRAMMES
  • JOBS AND SCHOLARSHIP
  • ANNOTED ATTRACTIONS
You are here : Home »
Showing posts with label tourism. Show all posts
Longido.jpg


Longido

The  tour  to  the  extensive  plains  around  longido  mountains, 80 km north  of Arusha, features  an  insight  into  the traditions of  Maasai  culture. The  lush  area  is  home  to  rare birds  and  animals.

The tour includes:

  1. A nature trail to spot birds
  2. A climb to the impressive Longido mountain through a dense natural forest 
  3. Walking safari through the Maasai plains and over the slopes of Longido mountain
  4. A visit to a traditional Maasai village
  5. A tour of historical sites dating back to British colonial times

 

Tour options: 
Half day tour
Longido  is  rich  in  birdlife.  Some  of  the  birds  seen  in  this  area starling  Major,  Red and Yellow Barbet,  Masked Weaver,  Silver Bill  and  Secretary  Bird. A  birdwalk  through  the Maasai  plains  starting  from  the town  of  Longido  to  the bomas  of  OI  Tepesi  allows  you  to see  birds  as  well  as trees  and  plants  used  by  the  locals  to  make  food  and  medicines. Later, visit  a  Maasai  boma  to see the  Maasai  lifestyle.  

Full day Tour

Add  to  th e birdwalk,  a walking  safari  from  OI  Tepesi  to  Kimokouwa  along  a  cattle  trail . Gradually  climb  to  an  altitude  of  1,600m  to  get  panoramic  views  of  Mt.Kilimanjaro  and Mt. Meru.  Descend  to  Kimokouwa's  green  "vallley  of  wells" and  nearby  historic  British  grave. On Wednesdays, you can extend your stay by visiting the bustling and colourful cattle market.
A  new  attraction  is a four day trekking trip -from Longido to the Big Rock and  Kitumbeine, on to  lake Natron.  

Longido mountain climb

Day 1

Walk  to  the  campsite  of  Kimokouwa  and   go  for  the  full  day  tour.

Day 2

Early  next  morning , follow  narrow  footpaths  through  dense  natural  forests  for  three  hours to  reach  the  beautiful  'dawa  ya  supu' or  medicine  soup  viewpoint. Another t wo  hours'  climb   leads  you  to  the  top  of  Longido  mountain  to  enjoy  fantastic  views  of  the other mountains  of   northern  Tanzania.  The descent  back  to  the campsite takes about  three hours. Finish  with  a  meal  with  the  FARAJA  women's  group.
 

 Where to stay


A good number of guest house is currently available within and around the town of Longido. Many more are in pipeline. Camping ground installed with modern toilet facilities is available. Arrangements for camping and hiring equipments and various activities of your interest will be organized by Local Tour Guides or coordination office. An option for staying in a Maasai boma for overnight can be smoothly organized. There are options for several days’ tour in the Maasai land and a long climb of Mount Longido for those doing exercise before trying to conquer the ‘Roof of Africa’ Mount Kilimanjaro.  Fly camping will be the best option.

Tour Guides:

The Local Guides are of the Maasai tribe and will guide you well in English and where necessary sign language will be used. They have good experience in guiding tourists in the area and deep cultural insight.

Various excursions and tours can be booked through Tanzania Tourist Board-Tourist Information Office in Arusha or through your tour operator/travel agent/lodge & Hotel Operator
 Getting there:
Longido is located about 80kms North of Arusha town. Its an hour drive via Arusha Nairobi high way. From the main bus stand in Arusha catch a bus or shared taxi leaving for Namanga and get off at Longido

(Income  f rom tourist visits will be used to improve the primary and secondary school classrooms,teachers' houses and water projects.)  

For further information contact:

Tell: +255 787 855185 /+255 27 2539209 / +255 715 855185

E-mail: touryman1@yahoo.comThis e-mail address is being protected from spam bots, you need JavaScript enabled to view it  

3 MAMBA MARANGU.JPG

1 MAMBA MARANGU.JPG

Mamba / Marangu

Mamba  and Marangu  in  the  Kilimanjaro  area  have  both  natural  and  cultural
heritage to offer the visitor. There are more  than  seven waterfalls  in the vicinity,
unique flora with tree, flower and  fruit nurseries  and  fauna.  Tour  the  slopes of
Mt.Kilimanjaro  and  ascend to beautiful viewpoints.
 
 
Tours  through  Marangu afford  panoramic  views of
Mt.Kilimanjaro. Visit  the  home  and  memorial  of  the
late  Yohana  Lauwo,  a Marangu native  who  accompanied
Dr.Hans  Meyer  on  the  first  recorded  climb  of  Kilimanjaro  in  1889,
and   read  the  original  log books of Lauwo.
Customised  half  day,  full  day  or  two  day  walking  safaris
can be  organised.  These  tours include  the  Kinukamori and
Moonjo  falls and a visit  to  a  Chagga  house  made  of
straw-roofing .  See  the  first  coffee  tree  planted  in
Tanzania and climb up  Ngangu  Hill.  A trip  to  the  African  Art  Centre
that  houses  a  collection  of  ancient  and  modern  sculptures, carvings
and  paintings  is  rewarding.
Mamba  is  a  paradise  for bird-watchers  and  nature  lovers.  Enjoy scenic
waterfalls,  tree, flower  and fruit nurseries,  pass  historical sites  the Laka
Holes-  large  hiding  caves  used  during  the  Chagga - Maasai  wars,
visit  a  wood  carving  school,  meet  a  local  blacksmith  using ethnic  methods
to  prepare  spears and tools, and  experience  Chagga  culture by  visiting a
traditional  Chagga  culture  by  visiting a  traditional  chagga  house.
Tour guides:
The guides of the Cultural Tourism Programme are of the Wachaga tribe who knows well the area, their culture & history and speaks English. Provision of outstanding customer service have been their life long way of life
Bookings for various excursions and tours can be made at Tanzania Tourist Board-Tourist Information Office in Arusha or through your tour operators/travel agents/lodge & Hotel Operators

Getting there:

Located at the foot of the’ roof of Africa’ one will catch a bus at Moshi town leaving for Marangu. Its a 45 minutes drive from Moshi town. Local Tour Guides will pick you at the bus stand on arrival. Mamba is located 3 kms from Marangu where walking or riding is possible. For those travelling from Dar-es-salaam will be supposed to get out at Himo Bust stand and then connect with mini-buses to Marangu.
Where to stay:
A wide range of Guest houses, lodges and hotels are available in Marangu and Mamba areas. A number of Homestay houses are available withing and around various villages bordering Kilimanjaro National Park. Camping ground installed with modern toilet facilities and clean water supply is available. Camping gears for hire at reasonable price are available in Moshi town
(Income from tourist visits will be used towards developing educational projects in the Kilimanjaro area)
For further information contact:
Tel: +255 754 818273/ +255 754 038265 / +255 754 390084 
email: marvellouscreation@mailcity.comThis e-mail address is being protected from spam bots, you need JavaScript enabled to view it
email: marvellouscreation@lycos.com
Sisikwasisi.jpg


Mbeya

Mbeya lies about 872 km south-west of Dar es Salaam, its landscape characterized by relief forms created by the volcanic effects of the African Rift Valley.

A visit to the region includes:

  1. A visit to the Ngozi Crater Lake
  2. A view into the traditional culture of the people of Mbeya
  3. Climbs to different mountain peaks in the area overlooking the East African Rift Valley
  4. Visit to the Mbozi Meteorite Stone and the Natural Bridge at Kiwira

  Different tours are on offer:

  Climb to Mbeya peak

Reaching the Mbeya peak (2,826m) is a steep climb taking about three hours. As you go along the mountain slopes, you see the indigenous flowers and colourful butterflies.

  Ngozi Crater Lake

Ngozi Crater Lake lies 38 km south of Mbeya, in the direction of Tukuyu and Lake Malawi. A narrow footpath winds uphill through  a dense tropical jungle full of bamboo and wild banana trees. Small mammals and colourful birds hide behind the thick vegetation. After a climb of one hour, you arrive at the crater rim for a magnificent view of the crater lake.

 Kiwira Natural Bridge and waterfalls

The Kiwira Bridge was created by the powers of a fast flowing river. Locals call this miracle ' Daraja la Mungu' or ' Bridge of God'. Worth visiting are the nearby Kijungu waterfalls.

 Rungwe Mountain climb

Rungwe Mountain at 2,960m is the highest peak in southern Tanzania. This volcano, active over the past million years, dominates the whole area around Tukuyu. It is a vast wild area, more than 100 sq km of forest, upland scrub and rock terrain, completely uninhabited and visited only occasionally. Take a long hike to the crater rim. 

 Matema beach

The 130 km drive from Mbeya to Matema beach is among the most scenic in Tanzania. A winding road passes through high mountains and tea estates before it descends to the tropical shores of Lake Malawi. From Matema, you can make canoe trips with fishermen over the lake to the nearby village where women specialise in pottery,and to the mouth of the river to spot hippos and crocodiles. It is also possible to organize hikes to the Livingstone Mountains.

 Mbozi meteorite and Sisi kwa Sisi farm

40 km south- east of Mbeya, lies the meteorite stone of Mbozi. This is the eighth largest meteorite in the world, weighing about 12 tonnes and dates back to atleast a thousand years. Nearby the stone, the Sisi kwa Sisi society is worth a visit to experience true African rural life.

 Other attractions

Several hot water springs, an underground crater known as 'bat caves', ruins of a 200 year old fort, Kaporogwe falls and Usangu basin are some of the other sites.
 

Where to stay

A wide range of guest houses, hotels and lodges is available in and around Mbeya city. Camping  grounds are available in various places including the urbun area, villages and the area  near or within Forests of the Southern Highlands at affordable rates. in Mbeya. Camping equipments are available at affordable rates in Mbeya. Coordination office or our  local tour guides will assist in making arrangements for home-stay and overnights in the villages, local gu est houses, lodges when making extended tours.

Tour guides

Our local tour guides were born and raised in Mbeya region.This gave then enough time to learn the life of the people, environment the culture & history of the area. They are trained guides who speak good English and will always provide to you an outstanding customer service during your visit.
Bookings for various excursions and tours can be made at Tanzania Tourist Board - Tourist Information Centre - Dar es salaam and Arusha or at Mbeya's Cultural Tourism coordination office located at ........ But also you can book through your tour operators/travel agent/ Lodge & Hotel operator

 

Getting There:

TMbeya is located in Southern highlands of Tanzania, about 10 hours tdrive from Dar es salaam. Daily bus transport is available but atleast one day before booking is appropriate.Train transport services by TAZARA can be another fairly good option. Mbeya is also linked with local charters.
(Income from tourist visits will be invested in agricultural projects of the Sisi kwa Sisi Society)

For furtherinformation contact:

Mbeya
Tel: +255 754 463471 /+255 754 087689

Email: sisikwasisitours@hotmail.comThis e-mail address is being protected from spam bots, you need JavaScript enabled to view it sisikwasisitours@hotmail.com


Jengo hili lilikuwa ofisi ya Mjerumani lakini sasa limegeuzwa kuwa hoteli
Na Charles Kayoka
Nilifika Wilaya ya Mikindani, mkoani Mtwara kwa mara kwanza miaka kumi na nne iliyopita. Nilipofika Mikindani kwa lengo la kuona majengo ya kihistoria niliona mengine bado yanaweza kukarabatiwa.

Katika safari hiyo nililiona boma la Mjerumani, ambalo lilionyesha kuwa ni kivutio kwa watalii wengi, lakini kasoro  iliyojitokeza halikuwa likitunzwa vizuri sana.Lakini ukienda leo hali ya jengo hilo siyo ile niliyoiona awali. Jengo limechukuliwa na wazungu walioligeuza kuwa hoteli. Kwa kweli linatunzwa vizuri sana. Na kilichofanyika ni kujitahidi kulirudishia kama lilivyokuwa awali. Linavutia na kwa kweli sio tena lile jingo chafu la Boma la Mjerumani kama unavyoyaona mengine ambayo hayatunzwi katika maeneo mbalimbali nchini.

Kutokana na hali hiyo nilijiuliza kwamba tunataka kutunza majengo yetu ya historia kwa kusubiri ufadhili kutoka nje tu!

Jambo la ajabu zaidi, Serikali imekuwa ikiwapa wananchi majengo ya kihistoria  amabayo wanayabomoa na kujenga ujenzi wanaoutaka. Historia inafutwa, kumbukumbu zinafutwa, na hakuna anayejali. Tumekaa tu!.
Serikali inazungumzia kuhifadhi na kukuza vivutia vya utalii. Ni utalii upi? Inasema kuwa inataka kuhimiza utalii wa ndani. Ni utalii upi?

Kama hata vivutio vilivyoko karibu na wananchi havitunzwi, tutawasaidia vipi watalii (wananchi) wa ndani ambao wamekuwa wakishindwa kutembelea mbuga zetu na vivuti vingine?
Tunapowaachia wageni uwezekano wa wananchi kufika katika majengo ya kihistoria ambayo yamegeuzwa kuwa hoteli ni mdogo kwa kuwa watahofia kuwapo kwa gharama kubwa  za kuingia hapo.

Nilifika Unguja na kutembelea makazi ya Sultan Seyd Barghash kuna makazi yaliyodumu kwa miaka zaidi ya mia sasa. Kuna miembe mingi yenye umri mkubwa sana tangu yalipopandwa na sultani huyo.

Nilidhani Serikali ingetafuta fedha na kuboresha bustani ya Unguja na kukarabati jengo la Barghash na kuweka huduma za buradani. Watalii na wananchi, na hasa wanafunzi, wangeweza kufika hapo na kujifunza mengi kuhusu historia ya taifa hili. Lakini jengo lile la Barghash linapotea na kuharibika kadri siku zinavyokwenda.

Kutokana na hali hiyo miaka 10 ijayo jingo hilo halitakuwapo. Nilifika Ras Mkambuu Pemba ambako kuna historia ya taifa tangu miaka mingi tangu Kuzaliwa kwa Yesu Kristo, historia inayotuunganisha na Wairan,(Washiraz kutoka Iran kusini), lakini majengo, makaburi, misikiti na visima vinapotea na siyo muda mrefu vitamezwa na maji ya bahari. Hakuna mtu anayejali.

Wahifadhi watakuambia wanahangaika kutafuta wafadhili kutoka nje ili wawasaidie kutunza historia ya Tanzania. Kweli wageni wanakusaidia kutunza historia ya Taifa!
Kutokana na hali hiyo tutaandika katika vitabu vyetu vya historia kuwa majengo hayo yalijengwa na wageni, na yakaokolewa na wageni. Kila jengo limeokolewa na wageni.

Historia ikiandikwa na wageni maana yake ni kwamba hatujui tunakotoka na wapi tunakokwenda.
source: mwnanchi.co.tz
WATAFITI wa mambo ya kale wanapofika eneo la Engaruka, mkoani wa Arusha hujiuliza, “kabila lililokuwa likiishi hapa lilikwenda wapi?”

Hata hivyo hadi leo hakuna mtu mwenye jibu sahihi hivyo kabila hilo liko kwenye orodha ya makabila yaliyopotea. Watu wa Engaruka walikuwa wakiishi kwenye bonde la ufa eneo
lililopo kati ya Ziwa Manyara na Ziwa Natroni karibu na Kreta ya Ngorongoro.

Inaaminika kuwa kabila hilo, liliishi eneo la Engaruka kuanzia karne ya sita lakini utafiti za
hivi karibuni zinaonesha kuwa waliishi eneo hilo kuanzia zama za chuma mwanzoni mwa karne ya 15.

Utafiti uliofanywa na wataalamu wa mambo ya kale na watafiti wa mambo ya akiolojia hususani John Sutton, unaonesha kuwa eneo la Engaruka lilikuwa na maelfu ya watu ambao waliishi katika mfumo wa vijiji na walikuwa wakiishi katika vijiji vikubwa saba na mashamba yao yalikuwa na ukubwa wa ekari 5,000.

Tafiti mbalimbali zinaonesha kuwa kabila hilo lilikuwa linajishughulisha na kilimo cha kisasa
cha umwagiliaji pamoja na ufugaji na inakisiwa kwamba lilitelekeza mashamba yao kati ya mwaka 1700 na 1750 na kuhama eneo hilo kutokana na sababu ambazo hadi leo hazijajulikana.

Urithi ulioachwa na kabila hilo ndio unaowafanya wanasayansi kuendelea kulitafuta kabila hilo bila kuchoka. Eneo lililotelekezwa lina miundo imara ambayo inadhihirisha kuwa watu wa kabila hilo walikuwa wakulima stadi wenye vipaji na utaalamu wa hali ya juu katika kilimo
cha mwagiliaji. Pia walifuga ng’ombe, mbuzi na kondoo.

Ingawa kabila hilo lilitoweka miaka mingi kabla ya kuingia zana bora za kilimo, lilikuwa linatumia mbinu bora za kilimo cha kisasa kwa kuwa katika makazi yao kulikuwa na mashamba yaliyotengenezwa kitaalamu kwa lengo la kuzuia mmomonyoko wa udongo.

Inasemekana watu wa Engaruka waliishi katika eneo tambarare lisilofaa kwa matumizi ya kilimo kwa kuwa lilikuwa na ukame na udongo mwepesi mithili ya vumbi jembamba. Hata hivyo, walitumia utaalamu wa hali ya juu na wa kipekee kutengeneza vitalu ambavyo kingo zake zilijengwa kwa mawe.

Pia walichimba mifereji kutoa maji sehemu zenye miinuko na kuyapeleka katika mashamba waliyoyatengeneza kwa ustadi mkubwa. Mirereji hiyo ilijengwa kwa kutumia mawe ili kuzuia maji yasipotee, na iligawanywa na kufanywa kuwa miembamba ili kusambaza maji kwenye mashamba.

Pia waliweka mawe kwenye kingo za matuta ili kuzuia mmomonyoko wa udongo. Waliokuwa wafugaji wa ng’ombe, mbuzi na kondoo walikuwa na utaratibu wa kuweka mifugo yao katika mazizi kisha kuitafutia chakula ili kuepuka mmomonyoko wa udongo unaosababishwa kulisha mifugo mingi katika eneo dogo.

Watu hao walikuwa wakitumia samadi kurutubisha mashamba hivyo walikuwa watunzaji wazuri wa mazingira. Kwa kuwa kabila hilo lilitoweka kabla ya kuanza kutumika kwa mfumo
wa kuweka kumbukumbu kwa maandishi, hakuna mtu anayefahamu watu hao walikuwa wa namna gani na walizungumza lugha gani.

Pia hakuna mwenye uhakika kama kabila hilo lilikuwa likijiita Engaruka. Watu waliofika eneo hilo waliamua kusema ni kabila la Engaruka kwa sababu eneo hilo lilikuwa likiitwa Engaruka.

Mwandishi wa Kitabu cha Makabila ya Kaskazini Mashariki mwa Tanzania, Gervase Mlola, anasema kuwa baadhi ya watu wanasema jina la Engaruka linatokana na asili ya neno la Kimaasai “ng’aruka” likiwa na maana ya sehemu kame au jangwa.

Inasemekana kuwa baada ya Wamasai kuhamia eneo la kusini, waliamua kuita eneo hilo Engaruka, kwa sababu walilifananisha na jangwa. Pia wapo wanaoamini kuwa jina la Engaruka linatokana na neno la kisukuma “Wangaruka”, ikiwa na maana salamu za asubuhi.

Inasemekana kuwa eneo hilo, lilikuwa kituo cha mapumziko cha Wasukuma, ambao walikuwa wakisafiri kutoka kanda ya Ziwa kwa ajili ya kukutana na wafanyabiashara waliokuwa wakitokea Mashariki.

Hata simulizi za Wasukuma hazioneshi kuwa waliwahi kukutana na watu wa Engaruka wakati wakiwa katika safari za kibiashara.

Mhifadhi Mkuu wa mambo ya akilojia katika Makumbusho ya Taifa na Nyumba ya Utamaduni, Amandus Kwekason anasema inaaminika kuwa kabila hilo lilitoweka na haijulikani liliko kwa sababu sio rahisi kabila linalokaa katika mfumo wa vijiji kubadilisha kabisa mfumo wa maisha na kuanza utamaduni mpya.

“Ingawa hivi sasa Wamaasai wanaishi eneo la Engaruka ni wazi kuwa Wamasai sio watu wa asili wa Engaruka kwa sababu sio wakulima. Wapo wanaodai kuwa kabila la Wairaqi linatokana na watu wa kale wa Engaruka lakini utafiti wa kisayansi unaonesha kuwa zana na
utamaduni wa kabila la Wairaq unatofautiana na ule wa Engaruka,” anasema Kwekason.

Anasema watu wanaoweza kubadilisha mfumo wa maisha ni watu waliotekwa na kupelekwa
utumwani kisha kuchanganywa na jamii nyingine na kulazimishwa kufuata mfumo na utamaduni wa watu wengine.

Hivyo inaaminika kuwa kabila la Engaruka lilitoweka kwa sababu zinazotokana na wao
wenyewe kwa kuwa Tanzania haina historia ya kabila nzima kutekwa au kupelekwa utumwani.
Kwekason anasema utafiti wa kina uliweza kukusanya vipande 5,280 vya masalia ya watu wa Engaruka ikiwa ni pamoja na mifupa na zana mbalimbali zilizotumika kwenye karne ya 15.

Masalia yamehifanyiwa katika Makumbusho ya Taifa na Nyumba ya utamaduni jijini Dar es
Salaam na hutumika kuendelea kufanya utafiti wa kutafuta kabila hilo kwa kuoanisha zana za watu hao na zana na makabila mbalimbali Tanzania na nchi jirani.

Pia utafiti umefanyika kwa kuangalia kwa kina miundo ya watu wanaojihusisha na kilimo cha umwagiliaji lakini hakuna mfumo inayofanana na ile iliyoachwa Engaruka. Ingawa wataalamu hawajajua sababu ya watu hao kuhama, kuna sababu mbalimbali zinazokisiwa.

Mosi inakisiwa kuwa huenda walikimbizwa na Wamaasai kwa sababu watu hao walitoweka karne ya 17 kipindi ambacho Wamasai walihamia maeneo ya Kusini na kufika eneo hilo la Engaruka.

Inakisiwa kuwa huenda watu wa Engaruka walihofia kwamba wageni waliofika na mifugo mingi wangeharibu mashamba yao jambo lililosababisha kuhama. Hata hivyo hakuna ushahidi
kwamba Wamaasai walivamia watu wa Engaruka kwa sababu katika simulizi za historia ya kale hakuna sehemu ambayo Wamasai wanataja watu wa Engaruka.

“Kwa kuwa historia ya kale ilikuwa ikihifadhiwa kwa njia ya simulizi, inaaminika kuwa Wamaasai hawakuwahi kukutana na watu wa Engaruka ndio maana simulizi zao hazitaji watu wahao,” anasema Kwekasoni ambaye pia ni mtalamu wa mambo ya akiolojia.

Pia ushahidi unaonesha kuwa wamasai wana uwezo wa kuishi na wakulima hivyo isingekuwa rahisi kwa watu hao kutoweka kabisa kwa sababu ya kugombana au kuhofia kuishi na wamaasai.

Wapo wanadhani kwamba watu wa Engaruka walitelekeza mashamba yao kutokana na
mabadiliko ya tabia nchi yaliyolikumba eneo la Kusini mwa Ikweta. Inasemekana kuwa
katika karne ya 15 na 16 mito inatiririka maji wakati wote ilikauka kutokana na ukame
uliojitokeza karne ya 17 na 18, kipindi ambacho watu hao walitoweka.

Hata hivyo, sababu ya ukosefu wa maji haijaweza kuthibitishwa kwa sababu bado kuna makabila mengine yanayokaa katika maeneo ya jirani kama Wasonjo na Wairaqi.

Wataalamu wa masuala ya mazingira wanasema mabadiliko makubwa ya mazingira yanaathiri jamii za watu wengi hivyo isingewezekana mabadiliko hayo kuathiri watu wa Engaruka pekee na kuacha makabila mengine yanayoishi karibu na eneo hilo.

Pia wapo wanaodai kuwa huenda watu wa Engaruka walikabiliwa na tatizo la ongezeko la watu hivyo waliamua kuhama kwa lengo la kutafuta ardhi kubwa ili kuendeleza kilimo cha umwagiliaji.

Hata hivyo, sababu hivyo imepingwa kitaalamu kwa sababu hadi leo hakuna anayefahamu walikokwenda.

Utafiti uliofanywa na Louis Leakey mwaka 1935, Hamo Sasson mwaka 1964, na mwaka 1966, Peter Robertshaw na Taasisi ya Uingereza mwaka 1982 unaonesha kuwa baadhi ya utamaduni wa watu wa Engaruka unafanana na wa Wanjo, kabila ambalo linaishi kilometa 100 Kaskazini mwa Ziwa Natron.

Kwa kuwa Wasonjo hawaishi mbali na Engaruka, baadhi ya watafiti walihisi kuwa Wasonjo wanatokana na watu wa kale wa Engaruka kwa kuwa wanajihusisha na kilimo cha umwagiliaji na muundo wao wa kutengeneza mifereji unashabihiana kidogo na ule wa Engaruka.

Hata hivyo, utafiti wa kina unabainisha kuwa Wasonjo hawana utaalamu wa kutumia mawe kuzuia mmomonyoko wa udongo. Pia hawatumii samadi kwa ajili ya kurutubisha mashamba yao.

“Kwa ujumla kilimo cha Wasonjo hakitumii mbinu za kisasa ikilinganishwa na kilimo
kilichokuwepo katika vijiji vya zamani vya Engaruka hivyo ni dhahiri kwamba Wasonjo sio
watu wa Engaruka,” inaeleza ripoti ya utafiti uliofanywa Sutton.

Jambo lingine linalodhihirisha kuwa Wasonyo hawatokani na kizazi cha kale cha Engaruka ni tofauti katika utengenezaji na matumizi ya vyombo hasa vyungu na mitungi pamoja na vyombo vingine vya ndani vilivyotengenezwa kwa kutumia udongo.

Baadhi ya watu walihisi kuwa huenda watu hao walihamia Kilimanjaro Magharibi. Wanasayansi wa masuala ya akiolojia walipiga kambi mkoa wa Kilimanjaro na kufanya utafiti wa kina. Utafiti huo ulibaini kwamba watu wa Kilimanjaro wana baadhi ya mambo yanayofanana na watu wa Engaruka.

Mosi, uhaba wa ardhi umesababisha Wachaga kutunza ardhi yao kama watu wa Engaruka na wanajihusisha na kilimo na ufugaji. Ufugaji wa Wachaga ni kama wa Engaruka, kwa sababu wanakabiliwa na uhaba wa ardhi.

Pia ufugaji wao ni kama wa watu wa Engaruka kwa sababu wanafuga mifugo michache ambayo hufungia kwenye mazizi kisha kuitafutia chakula. Pia wanatumia samadi inayotokana na mifugo hiyo kwa lengo la kurutubisha ardhi yao ya kilimo kama watu wa Engaruka.

Hata hivyo, wanasayansi walibaini kuwa ipo tofauti kubwa katika uandaaji wa mashamba kwa sababu pamoja na kuwa na maji yanayotiririka kutoka sehemu za miinuko, Wachaga hawana utaalamu wa kutengeneza mifereji ya kilimo cha umwagiliaji kama watu wa Engaruka.

Pia, vyombo na mapambo yao ni tofauti na yale ya watu wa Engaruka. Ingawa Wachaga wanakabiliwa na uhaba wa ardhi wamefanikiwa kwenda kutafuta maisha sehemu nyingine ila wana kawaida ya kurudi nyumbani kila mwaka kwa lengo la kudumisha mila na desturi zao, hivyo Wachaga hawana uhusiano na watu wa kale wa Engaruka.

Pia, utafiti kama huo ulifanywa katika jamii ya watu wa kabila la Wapare mkoani Kilimanjaro na katika milima ya Taita nchi ya jirani ya Kenya na matokeo yanaonesha kuwa kabila hilo ni tofauti na Engaruka.

Ufafiti huo ulibaini kuwa katika nchi ya Kenya kuna kabila la Marakweti ambalo mfumo wao wa kutengeneza mirefeji kwa kilimo cha umwagiliaji unashabihiana na ule wa Engaruka.
Kabila hilo linaishi kilometa 400 Kaskazini mwa Kenya katika bonde la Kerio.

Hata hivyo utafiti uliofanywa na Scotsman Thomson unaonesha kuwa kuna tofauti kati ya makabila hayo, hasa kwa kuangalia zana na mapambo yao. Watu wa Engaruka walikuwa
wakitumia shanga kutengenezwa mapambo, pia walivaa mikufu iliyotengenezwa vyuma vizito.

Pia walikuwa na mapambo machache yanayotokana na makasha ya wadudu wa baharini kama vile simbi. Vyungu na mitungi yao ilitengenezwa kwa ustadi mkubwa na katika mtindo tofauti na makabila mengine yaliyoishi jirani na Engaruka.

Ingawa kabila la Engaruka lilitoweka, liliacha urithi ambao unatumika na wanasayansi hadi
leo. Mfumo wao wa kilimo cha umwagiliaji ni kielelezo kuwa Waafrika wana utaalamu wa kijadi katika kilimo cha umwagiliaji na kwamba utaalamu huo haukuletwa na ukoloni.

Kutoweka kwa kabila hilo ni changamoto hasa kwa wanasayansi na watafiti wa mambo ya kale. Taarifa za tafiti mbalimbali zilizofanyika kwa zaidi ya miaka 100, hazijaweza kubaini watu wa kabila hilo wako wapi na kwa nini walitelekeza makazi yao ya asili.

Kutoweka kwa kabila hilo ni changamoto kwa makabila mengine ambayo yanaacha utamaduni wao wa asili.

Kwa kuwa binadamu ana shauku ya kujua asili yake ni vyema akabila kujitahidi kutunza kumbukumbu hasa kuwafundisha watoto lugha za asili, na kuweka rekodi za makabila hasa kipindi hiki ambacho Tanzania imeingia kwenye mfumo wa utandawazi ambao unasababisha watu wengi kuacha kutumia zana za asili na kutumia zana zilizotengenezwa na mataifa ya Magharibi.
more information visit: http://www.habarileo.co.tz/makala 
The Sukuma Museum is a community-based organization that promotes and celebrates the traditional and contemporary arts of the Sukuma culture. The Museum provides an interactive and educational environment where Sukuma elders teach younger generation traditional history and arts, and younger generations are encouraged to develop and expand creative voices and new Sukuma artistic trends.
Home
ADVERTISMENT
Sanya Consultant Company; deals with project proposal writing, conducting ESIA in different projects, research proposal writing.

contact: +255789606882

LISTEN RADIO FREE AFRICA LIVE

Most viewed Contents

  • TCU Guide book - Kwa wanaoomba vyuo 2012/2013
  • Engaruka:Kabila lililotoweka kimiujiza
  • WASHIRIKI WA BIG BROTHER FROM TANZANIA HAWA HAPA
  • Mbeya
  • Mamba / Marangu
  • MAIGE: "NAPE NI GAMBA"
  • MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA CHETI NA STASHAHADA 2012/2013
  • DIAMOND: "NAMSHUKURU WEMA SEPETU KWA KUNIFUNDISHA KIINGEREZA"
  • Boma la Mjerumani Mikindani ni kivutio
  • Bujora Museum

Utalii Tanzania On facebook

football online

Footbal Updates

Get Adobe Flash player
live scores

Online Visiters

© 2012 - Utalii Tanzania. All rights reserved.

Designed by Mhoja L. Matandiko

hit counter